Thursday, May 9, 2013
VIDEO : POLISI AKUTWA NA KICHWA CHA BINADAMU ALICHOKUA ANATAKA KUMSAKIZIA MFANYABIASHARA
WATU wanne wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Morogoro akiwemo askari polisi watatu wa jeshi la polisi mkoani Morogoro na raia mmoja kwa kuhusishwa na tuhuma za kumbambikizia tuhuma za kukutwa na kichwa cha binadamu mfanyabiashara wa mjini Dumila wilayani Kilosa mkoani hapa.
Wakizungumza na Clouds Tv wananchi wa mtaa wa Mgudeni Dumila wilayani Kilosa akiwemo mwenyekiti wa mtaa huo Zaituni Kifutu,MOhamed Fungafunga na Musa Magisu wanasema tukio hilo ni la kushangaza ambalo limetokea leo na kwamba polisi kwa kushirikiana na raina mmoja wanadaiwa kubambikizia tukio hilo mfanyabiashara wa eneo hilo Samson Mura ambapo walimtaka kutoa shilingi milioni ishirini na tano ili waweze kumwachia kitendo ambacho alikipinga.
kwa upande wake afisa upelelezi msaidizi wa polisi mkoa wa Morogoro Asifiwe Ulime amekiri kutokea tukio hilo na alifika eneo la tukio na kushuhudia fuvu hilo ambapo alisema kuwa askari hao watatu akiwemo na mwananchi huyo mmoja wanashikiliwa na jeshi la polisi ili watoe maelelezo ya kina na kuwaomba wananchi wa Dumila kuwa watiulivu wakati uchunguzi unaendelea.
Comments System
facebook