Thursday, February 12, 2015

WAKONGWE MISS ELIOT NA TIMBALAND WARUDI STUDIO



Unapozungumzia gemu la muziki aina ya hip hop hususani kwa wakina dada, huwezi kuacha kumtaja mkongwe Miss Eliot, watu wengi hasa mashabiki wake walikuwa wakimuombea siku moja arudi studio na kufanya ngoma, mara ya mwisho alifanya show wakati wa Superbowl 49, hilo liliwapa tumaini mashabiki kwamba kuanzia pale angerudi studio na kupiga kazi.

Miss Eliot amepost kupitia ukurasa wake wa twitter akionekana n mtayarishaji aliyekuwa akifanya nae kazi kwa karibu mkali Timbaland, kwenye picha wameonekana wako bize studio.


Lakini katika picha hiyo hapakuwa na maelezo yeyote, tunajiuliza wenyewe, tunawaza kwa sauti je Eliott anatengeneza albamu mpya au Timbaland anafanya kazi kwa ajili ya wasanii wake wengine? Tusubiri tuone endapo Miss Eliot na Timbaland baada ya kutofanya kazi kwa muda mrefu kama ni kweli tutaona inakuwaje kwa sababu sasa hivi kuna Iggy Azalea,Nick Minaj, Miley Cyrus na wengine wakali atarudije tusubiri…

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.