Tuesday, April 28, 2015

WATUHUMIWA WA DAWA ZA KULEVYA KUPIGWA RISASI LEO

Raia wa Australia Andrew Chan (kushoto) na Myuran Sukumaran wanaosubiria kuuawa kwa kupigwa risasi kesho asubuhi nchini Indonesia.
Dada wa Sukuraman, Brintha, akisaidiwa na watu kuelekea bandarini wakati akienda kumuaga kaka yake kwa mara ya mwisho kwenye Kisiwa cha Nusakambangan.
Michael Chan (katikati mwenye tisheti ya kijani) ambaye ni kaka wa Andrew Chan, akikatiza kwa wanahabari kuelekea bandarini tayari kwenda kumuaga kaka yake.
Majeneza ya Chan na Sukuraman yakiwasili katika Kisiwa cha Nusakambangan.
Mama mzazi wa Sukuraman, Raji (katikati), akilia kwa simanzi wakati akiwasili katika bandari ya Wijaya Pura kuelekea Kisiwa cha Nusakambangan kumuaga mwanaye.
Wanahabari wakiwazingira wanafamilia wa Chan na Sukumaran ili kupata picha za matukio.
Brintha Sukumaran ilibidi abebwe baada ya kuwasili katika gereza lililopo Kisiwa cha Nusakambangan.
Sukumaran (kushoto) na Chan (kulia) watapatiwa nguo nyeupe kabla ya kupigwa risasi na watachagua iwapo wapigwe risasi wakiwa wanaangalia au wafunikwe sura zao. Tayari Sukumaran ameomba kuuawa akiangalia.
VIGOGO wawili katika sakata la kutaka kusafirisha dawa za kulevya aina ya heroin kutoka nchini Indonesia, Andrew Chan na Myuran Sukumaran wanatarajia kuuawa kwa kupigwa risasi kesho Jumatano asubuhi.
Familia za vigogo hao jana zilitawaliwa na simanzi wakati zikiwaaga kwa mara ya mwisho wapendwa wao hao waliopo katika gereza moja kwenye Kisiwa cha Nusakambangan nchini Indonesia.
Majeneza ya Chan na Sukumaran tayari yamepelekwa katika kisiwa hicho kinachojulikana kwa jina maarufu la 'death island' likimaanisha kisiwa cha kifo.
Andrew Chan na Myuran Sukumaran walikuwa viongozi wa kundi la watu tisa walionaswa wakitaka kusafirisha kilo 8.3 za dawa za kulevya aina ya heroin zenye thamani ya zaidi ya bilioni 6, Aprili 17, 2005 huko Denpasar, Bali nchini Indonesia. Kundi hilo lilipewa jina la Bali Nine.
Kundi la Bali Nine lilikuwa likiwahusisha raia wa Australia tisa ambao ni Andrew Chan, Si Yi Chen, Michael Czugaj, Renae Lawrence, Tan Duc Thanh Nguyen, Matthew Norman, Scott Rush, Martin Stephens na Myuran Sukumaran.
Mwaka 2006 watuhumiwa saba kati ya tisa walihukumiwa kifungo cha maisha jela huku Andrew Chan na Myuran Sukumaran wakihukumiwa kuuwa kwa kupigwa risasi.

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.