Friday, September 9, 2016

Msafara wa Makamu wa Rais wapata ajali mkoani Mtwara.

Kwa mujibu wa mashuhuda,watu 4 wamejeruhiwa baada ya gari moja katika msafara wa Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan kupata ajali na kupinduka eneo la Nanguruwe wakati msafara huo ukitokea mkoani Mtwara kuelekea Tandahimba ambapo majeruhi wa ajali hiyo wamepelekwa katika Hospitali ya Mkoa wa Mtwara, Ligula.



Makamu wa Rais yupo mkoani Mtwara katika ziara ya kikazi ya siku nne ambapo pamoja na mambo mengine amefungua ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kusini hafla
iliyofanyika mkoani Mtwara.

                             Makamu wa Rais,Mama Samia Suluhu Hassan.

Tutaendeleea kufatilia taarifa hizi kwa undani na kuwahabarisha.

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.