Friday, September 9, 2016

VIDEO: Tazama alichofanya Shilole kwa Nuh Mziwanda @Fiesta Tour Tabora.

Tamasha la Fiesta linaendelea kuzunguka kwenye mikoa mbalimbali ambapo leo ni zamu ya wakazi wa mkoa wa Tabora kuwashuhudia wasanii mbali watakaolishambulia jukwaa la Fiesta Mkoani humo ambapo mbali na list ndefu ya wasanii watakao-perfom mkoani humo,gumzo kubwa litakua ni wapenzi wa zamani Nuh Mziwanda ambae kwa mara ya kwanza atakutana stejini na aliekua mpenzi wake Shilole maarufu kama "Shishi baby".

Tofauti na watu wengi walivyotarajia,video fupi iliyosambaa mtandaooni imewaonesha wapenzi hao wa zamani wakikumbatiana wakiwa kwenye bus la wasanii hali iliyoamsha shwangwe miongoni mwa wasani wenzao.



Nuh Mziwanda anatamba na hit's yake ya "Jike Shupa" ambayo inadaiwa amemuimbia Shilole mara baada ya mapenzi yao kufika tamati wakati Shilole akisumbua na hit's yake ya "Mtoto Mdogo" ambayo mashairi yake yameakisi mahusiano yake na watu aliowazidi umri akiwemo Nuh Mziwanda.

Swali la kujiuliza je wawili hawa watapanda jukwaani pamoja hasa ikizingatiwa kuwa Tabora ndio mkoa anaotoka Shilole.Nadhani mashabiki wa Mkoa huu wata-enjoy kitu cha tofauti zaidi.

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.