Wednesday, December 14, 2016

PICHA:Yaliyojiri kwenye ukaguzi wa Polisi kwenye ofisi za Jamii Forum na nyumbani kwa Mkurugenzi wa mtandao huo.

Mnamo tarehe  14 Disemba mchana  Polisi kutoka kituo cha Kati, Dar es salaam wakiambatana na Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Jamii Media,inayomiliki mtandao wa 'Jamii Forum' Ndugu Maxence Melo, walifika katika ofisi za Jamii Media kwa ajili ya ukaguzi.

Zoezi hilo lilienda sambamba na kuwahoji wafanyakazi (Social Media Engagers na Content Quality Controllers) juu ya utendaji wa shughuli zao za kila siku ndani ya ofisi za kampuni hiyo zilizopo Mikocheni jijini Dar es salaam na kuondoka na  wafanyakazi wawili kwa mahojiano zaidi ambapo walielekea nyumbani kwa Maxence Melo kwa ajili ya ukaguzi ndani ya nyumba.
Katika zoezi zima la ukaguzi, sehemu zote mbili, Jeshi la Polisi halikuhitaji wala kuchukua kifaa cha mawasiliano ya kimtandao kama router, flash, hard disc, au kompyuta ila walichukua baadhi ya nyaraka za usajili wa kampuni hiyo.

Eneo la nnje la nyumba ya Maxence Melo.
 

Hata hivyo baada ya ukaguzi huo kwenye nyumba ya Bwn.Melo,msafara huo ulielekea kituo cha kati kukamilisha mahojiano kati ya Mkurugenzi huyo na wafanyakazi wawili waliochukuliwa.

Credit:Mashuhuda wa SHILAWADU.

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.