Tuesday, August 5, 2014

YOU HEARD: PENZI LA SHILOLE NA NUH MZIWANDA LAVUNJIKA

Nuh Mziwanda na Shilole Enzi za Mahaba yao
Siku ya jana haikua nzuri kwa Shilole na Nuh Mziwanda baada ya kugomabana sana hadi Nuh Mziwanda akaamua kuchukua vitu vyake na kuhama Kwa Shilole, Gazeti la Makorokocho imezipata taarifa hizi za motomoto kupitia kwa mtu aliyekuepo eneo la tukio aliyedai kuwa yeye alishangaa kuskia mikikimikiki ndani ya Harrier na baadae milango ya gari ikafunguliwa wakatokeza wasanii wawili wa bongo flava ambao ni Shilole na Nuh Mziwanda na walikua wakirushiana maneno ghafla wakatokeza watu wengine wakiongozwa na Msanii Chege Chigunda wakaamulizia ugomvi huo bila Mafanikio kwani Nuh Mziwanda alikua anamuambia Shilole amrudishie simu yake lakini Shishi alishindwa kufannya hivyo kwa madai eti ufunguo upo nyumbani, Kweli? wakati dakika chache zilizopita walikua ndani ya Gari
Nilipomtafuta Nuh Mziwanda hakutaka kubisha na akatiririka A to Z ya sakata hilo,
Nuh Mziwanda: Jana Usiku tulialikwa Chakula Usiku kwa Producer Dibanjo, mitaa ya Mango Garden Kinondoni, mimi na Shilole tulipofika pale tukamkuta mwenyeji wetu pamoja na wasanii wengine Chege, Julio, Dully Sykes na wengine, ikafika muda nikawa sijiskii vizuri nikamuomba Shishi funguo ya gari ili nikapumzike kwenye gari, kufika kule nikazikuta simu za Shilole zikiwa na misscall nyingi pamoja na msg, nikazikagua na kukuta msg ya mwanaume akimwambia Shilole "Nimeingia Dar" .... ikabidi nimuite Shilole na kumkaripia sana Shishi akajitetea kuwa yule si bwana wake, Nikamwambia sawa mpigie niskie maongezi yenu, lakini Shishi alipompigia sikuelewa maongezi ndo nikamzaba kibao cha nguvu na Shishi akajibu mapigo kwa kuning'ata mwilini pamoja na kidole changu kimevimba mpaka wakati huu, watu wakajaa eneo la tukio hadi kina Chege wakafika na kuanza kuamulizia tukaacha kupigana lakini mwisho wa siku Shilole alikua amenipokonya simu yangu nilipomuomba akakataa kuirudisha na kuondoka eneo la tukio,  Ikabidi na mimi nisepe kwenda Nyumbani kwa Shilole ambako nilikua naishi nae ila nia yangu ilikua ni kwenda kuchukua vitu vyangu ili nihame nyumba ile, njiani karibu nafika nikakutana na vibaka wakaniibia mpaka viatu, nikaendelea na safari lakini nilipofika pale kumbe Shishi alikua amempigia simu Dada wa Kazi asinifungulie mlango, ikabidi nikae hapo nje weeee mida mida Shilole akafika na kupitiliza ndani akajifungia mimi nikiwa nje, asubuhi wakajisahau na kuacha mlango wazi ndipo nilipopata upenyo nikaingia na kuchukua laptop, guiter pamoja na nguo vyote vyangu na kumwachia nyumba yake.

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.