Wednesday, February 11, 2015

MASTAA 11 DUNIANI WALIOKUFA KWA AJALI ZA MAGARI



Paul Walker aliacha dunia na Hollywood katika mshituko kufuati kifo cha ghafla, muigizaji huyo star wa movies ya Fast & Furious alifariki Novemba 2013. Paul Walker alifariki akiwa na umri wa miaka 40 akiwa baba wa mtoto mmoja, alikufa kwa ajali mbali mbaya ya gari akiwa anaendeshwa na rafiki yake Roger Rodas wakiwa na gari aina ya 2005 Porsche Carrera GT. Gari iligonga nguzo ya taa na kuwaka motoa Paul Walker alifariki hapo hapo.

Ryan Dunn baada kuweka maisha yake matatani baada ya kufanya utani mmbaya kupitia TV, star huyo mwenye vituko Ryan Dunn alikufa kwa ajali ya gari baada ya Porsche 911 ilipotoka nje ya barabara huko Pennsylvania 2011.
Taarifa za polisi ziliripoti kwamba star huyo aliyekuwa na miaka 34 alikuwa amezidisha mara pindi kiasi cha pombe kinachoruhusiwa kisheria alikuwa akiendesha speed ya 130 mph ndipo gari ikapata ajali na kuwaka moto, Wote Ryan Dunn na abiria Zachary Hartwell aliyekuwa kwenye gari walikufa .
 


James Dean  kama ungekutwa ndani ya gari yake aina ya Porsche Spyder 550 huwezi toka ilikuwa ajali mbaya, aligongana na gari nyingine ambayo ilikuwa ikikatiza mbele yake,alikufa baada ya kuvunjika shingo, James Dean alifariki akiwa na miaka 24 tu ilikuwa Septemba 1955.
Maisha ya Princess Diana yalikatizwa Agosti 1997 pale gari aliyokuwa akiendesha iligonga nguzo za pembeni za barabara za chini huko Paris. Princess Diana majeraha aliyokuwa ameyapata akafariki baadae hospitali, sio Diana wala aliyeongozana nae, Bwana Dodi Fayed alikuwa amefunga mkanda wakati wakipata ajali hiyo. Wakati huo huo dereva aliyeitwa Henry paul ambae paia alikufa alikutwa na kiasi kikubwa cha pombe katika mwili wake.
Grace Kelly miaka 15 kabla ya kifo cha Princess Diana, Princess Grace wa Monaco alihusika katika ajali mbaya ya gari Septemba 1982. Muigizaji huyo wa Hollywood alipata stroke wakati akiendesha gari yake aina ya Rover, gari ikaanguka ina kubiringita mita 120 chini ya bonde, Grace aliyekuwa na miaka 52 alikufa kutokana na majeraha siku iliyofuata . Princess Stephanie ambae nae alikuwa ndni ya gari  alipona.
Lisa “Left eye” Lopez ajali mbaya iliyotokea huko Honduras ilikatiza maisha ya mwanamuziki kutoka kundi la TLC Aprili mwaka 2002. Left Eye alifariki akiwa na umri wa miaka 30, alikuwa katika kipindi cha mapumziko. Lopez alikuwa akiendesha gari akagonga miti miwili na gari kupinduka baada ya kulikwepa gari lingine alilokuwa agongane nalo.
Jayne Mansfield Law & Order: Star Mariska Hargitay alikuwa na bahati kuokoka kutoka katika ajali mwaka 1967 ajali iliyomchukua mama yake Jayne. Mansfield alikuwa ni abiria akiwa katika kiti cha mbele wakiwa na gari aina ya Buick Elecktra 225 ya mwaka 1966, waligonga tela ya trekta kwa nyuma huko Louisiana. Hargitary ambae alikuwa na umri wa miaka mitatu tu alikuwa amekaa nyuma na ndugu zake wawili ambao wote walipona.
Marc Bolan muimbaji wa rock wa Uingreza, alifariki Septemba 1977 baada ya gari yake aina ya Mini 127GT ambayo mchumba wake Gloria Jones alikuwa akiendesha iliingia kwenye ukingo huko kusini mahgaribi mwa London. Bolan ambae alikuwa na umri wa miaka alikufa papo hapo, taarifa zilieleza kwamba Bolan hakujifunza kuendesha gari kwa sababu hakupenda kufa mapema.
Dottie West muimbaji wa muziki wa Country,alikuwa amechelewa katika party ya Grand Ole Opry, ndipo gari aliyokuwa ndani yake ikapata ajali wakati akielekea eneo la tukio. Jirani yake ambae alikuwa akiendesha gari alishindwa kuicontrol gari ikapinduka. Dottie alipata majeraha ya ndani ikiwa ni pamoja na maini, alikufa siku chache mbele Septemba 4, 1991.
Randy  “Macho Man” Savage, ulimwengu wa mieleka ulipoteza star wake Mei 2011, alifariki kwa mshtuko wa moyo akiwa kwenye gari yake. Taarifa za Florida Highway Patrol, Savage alikuwa na umri wa miaka 58, akiwa kwenye Old Jeep Wrangler iligonga mti, mke wake Lynn ambae alikuwa kwenye gari alipona lakini Savage alifariki kutokana na majeraha.
Sam Kinison, ni mchekeshaji maarufu, alikuwa na umri wa miaka 38 wakati alipofariki baada ya gari aina ya pick-up truck kupata ajali na gari hiyo aliyokuwa akiendesha. Muhubiri huyo wa zamani ambae alifariki wakati akiendesha akitokea nyumbani kwake California kuelekea kwenye show yake ambayo tiketi zilikuwa zimeuzwa na kuisha (sold out) huko Laughlin Nevada, alipata tatizo linalojulikana kama dislocated neck na majeraha mengine. Ni kijana mwenye umri wa miaka 17 aliyekuwepo ndani ya agri hilo katika viti vya nyuma alikuwa akinywa pombe.
 



Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.