Wednesday, September 7, 2016

Baada ya tetesi za kuchepuka,Usain Bolt amvisha pete mrembo huyu.

Kwa wale warembo waliokua na ndoto kwamba siku moja wanaweza kuwa mapenzini na Mwanariadha mwenye kasi zaidi ulimwenguni Usain Bolt,ndoto zao tunaweza kusema zimeyeyuka kwani raia huyo wa Jamaica (30) kupitia mtandao wa Snapchat amepost video fupi inayomuonesha akiwa na mpenzi wake wa siku nyingi Kasi Bennett  kwenye fukwe za Bora Bora nchini Ufaransa,katika picha iliyoambatana na "emoj's" na maneno yanayosomeka "she said yes" ambapo kwa mujibu wa dada wa mwanariadha  huyo picha hiyo inamanisha mrembo huyo ameridhia kuvishwa pete na Bolt baada mahusiano yao kukumbwa  na mgogoro.


Kwa mujibu wa dada wa mwanariadha huyo,Christine Bolt-Hylton (32) amedai kuwa wawili hao kwa sasa wamemaliza tofauti zao na wanaonekana kupendana zaidi.."I'm sure Kasi will be used to it by now....."She is used to seeing pictures like this".."People ask for pictures with him and he is always willing to have pictures".. "She is used to him being in the public domain."

  Hata hivyo tetesi za Bolt kumvisha Bennet pete ya uchumba zimekuja mara baada ya wawili hao kuingia kwenye mgogoro baada ya picha za faragha  za  mwanariadha akiwa na binti mwanafunzi raia wa Braazil Jady Duarte (20) kusambaa  kwenye mitandao ya kijamii mara baada ya kumalizika kwa michuano ya Olimpiki iliyofanyika jijini Rio nchini Brazil.

Picha iliyosambaa kupitia mtandao wa whatsaap na kuleta mtafaruku kwenye mahusiano ya wawili hawa.

Mpaka sasa Usain Bolt ndie binadamu mwenye kasi zaidi ulimwenguni,huku akiweka na kuzivunja rekodi zake mwenye ambapo katika michuano ya Olimpiki iliyofanyika nchini Brazil mwaka huu amekua Mwanariadha wa kwanza kuweka rekodi ya kushinda medal tatu za dhahabu,mita 100,mita 200 na mita 100 reley.



Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.