Rais
wa Jamhuri ya Demokrasia ya Congo Joseph Kabila, amewahakikishia raia
wake kwamba ataheshimu Katiba ya nchi na kwamba hatawania urais katika
Uchaguzi mkuu ujao unaotegemewa kufanyika mwaka 2018.
Akilihutubia Bunge la nchi hiyo, Rais Kabila ameomba kuwepo amani na utulivu.
"Kwa wale ambao wanaingilia kati maisha yangu ya siasa kila siku,
ninasema asante lakini wafahamu ya kwamba Jahmuri ya Kidemorisia ya
Congo ni nchi inayoongozwa na katiba hatujakiuka katiba na tutaendelea
kuiheshimu. Kwa mda huu kilicho muhimu ni kuangalia maisha ya
wakongomani" Alisema Kabila.
Jana waziri mkuu Augustina Matata Ponyoa alijiuzulu kutoa nafasi wadhifa huo kuchukuliwa na upinzani kwenye utawala wa mpito.
Hatua hii ni ya kutuliza msukosuko wa kisiasa nchini DRC baada ya vyama vikuu vya kisiasa kususia mazungumzo ya kitaifa.
Chanzo:BBC.
