Friday, January 2, 2015

Wastara Asoma Dua Kumuenzi Sajuki aliyefariki siku kama ya leo.



Mwigizaji wa filamu za Kibongo Wastara Juma leo amesoma dua  maalumu kama ishara ya kumkumbuka na kumuenzi aliyekuwa mume wake kipenzi , marehemu Juma Kilowoko ‘Sajuki’.



Marehemu Sajuki alifariki dunia Januari 2.2013 , ambapo leo ametimiza miaka  miwili, dua ya kumuombea ilianzia katika makaburi ya Kisutu, jijini Dar es Salaam ambapo marehemu Sajuki alizikwa na baadae kuhamia nyumbani kwake Tabata.
Akizungumza na GPL, Wastara alisema anajisikia faraja sana kusoma dua kwa ajili ya mtu aliyempenda lakini pia anawashukuru wadau na  wote waliojitokeza katika kufanikisha  kisomo hicho.
Aidha wasanii mbalimbali wamejitokeza akiwemo Mohamed Mwikonge ‘’Frank’ Mtitu, Nisha, Bond na wengineo ambao pia wameomba na kuwakumbusha wasanii na wadau mbalimbali kuwakumbuka na kuwaenzi wasanii pindi wanapoaga dunia.

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.