Friday, September 2, 2016

Pep Guardiola amtosa Yaya Toure.

Kiungo mchezeshaji raia wa Ivory Coast,Yaya Toure ameachwa kwenye kikosi cha Manchester City kitakachoshiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu huu hii ikiwa ni mara ya pili kwa Kiungo huyo kuwa chini ya kocha Pep  Guardiola aliewahi kuwa Manager wake wkati akiitumikia Club ya Barcelona na kupata wakati mgumu kabla ya kuamua kuondoka na kuhamia Manchester City.
 Tayari Guardiola ameshawatoa kwa mkopo wacgezaji kama Joe Hart, Samir Nasri, Wilfried Bony na Eliaquim Mangala na kuleta mtikisiko kwenye klabu hiyo yenye maskani yake kwenye dimba la Etihad huku Toure akibakia klabuni hapo baada ya dirisha la usajili kufungwa juzi usiku.
                                  Yaya Toure (kulia) na Kocha Pep Guardiola.

Toure  mwenye umri wa miaka 33  alicheza dakika zote tisini kwenye mchezo wa raundi ya pili wa kufuzu kucheza hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Steaua Bucharest, lakini jina lake halijajumuishwa kwenye kikosi hicho kinachoundwa na wachezaji 21 ambapo Wachezaji wapya kama Claudio Bravo, John Stones, Ilkay Gundogan, Leroy Sane na Nolito wote wamejumuishwa kwenye kikosi hicho kitapambana na vilabu vya Barcelona, Borussia Monchengladbach na Celtic kwenye Kundi C.

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.