Wolper |
Mwanadada Star wa Bongo Movie, Jackline Wolper hivi karibuni amelalamika kuwa kuna matapeli wamei divert namba yake ya simu, hivyo simu zake
zote anazopigiwa zinaingia kwa huyo tapeli ambaye amekua akiwaomba watu hela
huku akijifanya yeye ndiye Wolper na amepatwa na tatizo,
Jacline Wolper anasema alishtukia mchezo huo baada ya
kusafiri kwenda South Africa kwa ajili ya matibabu, akapokea simu kutoka kwa
manager wake akimwambia kuwa kuna mtu huku bongo kaichakachua line yako ya simu
na anapiga vibomu a.k.a mizinga kwa watu ile mbaya, anasema ilibidi awahi
kurudi mwezi uliopita ili kufatilia ishu hii kwa ukaribu lakini kwa bahati
mpaka leo bado hajafanikiwa kumkamata mwizi wake.
Skiza alichoongea Jackline wolper hivi karibuni kwa hisani ya XXL ya Clouds
fm: