Sunday, September 4, 2016

Mitaa ya Jiji la Arusha kulindwa kwa CCTV-Camera.


MKUU wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, amesema kuwa ofisi yake  inakusudia kuimarisha usalama wa mkoa huo  kwa kufunga kamera za  CCTV zitakazosaidia kubaini matukio ya uhalifu na wahalifu kwenye mitaa ya Jiji hilo la kitalii.
             Sehemu ya mitaa ya Jiji la Arusha kama inavyoonekana kupitia picha ya satelite.

RC,Gambo amedai kuwa tayari  mchakato wa kutekeleza mpango huo umeanza  alipokua akizungumza na  na Balozi wa Sweden nchini, Katarina Rangnite , akiwa na ujumbe wa wabunge kutoka nchini humo,uliomtembelea ofisini kwake.
 Mkuu wa Mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo (kulia) akipokea zawadi kutoka kwa kiongozi wa ujumbe wa wabunge wa Sweden  Bi. Matilda Irnkarns waliomtembelea ofisini kwake.

           
"Tunakusudia kuongeza usalama mkoani mwetu kwa kufunga kamera za CCTV zitakazotuonesha matukio ya uhalifu na wahalifu watakaokuwa wakiwasumbua wananchi wa Arusha, watalii na hata wawekezaji Mkoani mwetu,"......"Tunapokuwa na uhakika wa kudhibiti wahalifu tunakuwa na uhakika wa usalama na kuwavutia watalii na wawekezaji,pia wananchi wanakuwa na amani,"Gambo alisema.


Kwa upande wake, Balozi Rangnite alikubali kuwekeza katika mfumo huo wa CCTV unaotegemewa kufanya kazi kwa saa 24 kila siku,na kuongeza  kuwa Sweden ina wataalamu waliobobea katika mifumo hiyo ya usalama wa miji hivyo kumuomba Mh. Gambo awasilishe ombi lake kwa maandishi mradi huo utekelezwe.

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.