Sunday, May 5, 2013

SHUJAA ALIYEMKAMATA ALIYELIPUA BOMU KWENYE KANISA ARUSHA ATIRIRIKA PICHA NZIMA ILIVYOKUA

Jana asubuhi jiji la arusha lilipata mshtuko mkubwa na simanzi nzito baada ya kutokea kwamlipuko wa mabomu uliotokea katika kanisa la kikatoliki huko olasisti nakupelekea vifo na majeruhi kwa baadhi ya waumini waliohudhuria katika sherehe ya ufunhuzi wa kanisa.. 

CHANZO..
Haya nimaelezo ya kijana aliyedai kuwa alishuhudia tukio hilo.
Kijana huyo(chini pichani aliyevalia tisheti ya njano) ametueleza kwamba bomu hilo lilirushwa na kijana mmoja ambaye kimwonekano alikuwa nikijana wa miaka 20-25. alizidi kueleza kwamba baada ya kijana huyo kurusha bomu alikimbia huku akiita MWIZI MWIZI MWIZI..


Eneo bomu lilipoangukia likiwa limezungushiwa utepe na jeshi la polisi
Baadhi ya mejeruhi

Kutoka na majeruhi kuwa wengi hospitali hadi vitanda vya wodi kuto kutoshea, ilibidi wasamaria wema wajitolee magodoro, kama unavyomuona muendesha pikipiki ya miguu mitatu akiwa amebeba magodoro hayo tayari kwa ajili ya kuyawahisha hospitali


Raia wakiwa wamejikusanya eneo la tukio
KUKAMATWA KWA MTUHUMIWA..
Kwabahati nzuri tulipata maelezo kutoka kwakijana ambaye alishirikiana na wananchi wengine kumkimbiza mtuhumiwa kutoka olasiti hadi katika kijiji kiitwacho ndorobo.. kijana huyo(mtizame mwisho kabisa katika post hii) alizidi kutueleza ya kuwa mtuhumiwa alikimbia kisha alijilaza katika miwa ila walisaidia na mbwa waliokuwa wakimkimbiza mtuhumiwa huyo.. mara baada ya kumkamata walimkuta akiwa na mfuko wenye bomu zilizobakia.. dakika chache wananchi wenye hasira kali walifika eneo alipokamatiwa mtuhumiwa huyo wakiwa na silaha kali za jadi wakitaka kumuua kijana huyo ndipo polisi waliokuwa wakisaidia na wananchi hao walifika eneo lile nakumchukua mtuhumiwa huyo.. 

HUYU NIMMOJA KATI YA VIJANA WACHACHE KABISA NINAOWEZA KUTHUBUTU KUSEMA NIKIJANA SHUPAVU ALIYEWEZA KUMKIMBIZA MTUHUMIWA NA KUMKAMATA AKISHIRIKIANA NA WANANCHI NA POLISI..
 hapa akielezea tukio zima lilivyotokea na jinsi walivyomkamata mtuhumiwa  
Posted by : David Mollel on :Sunday, May 5, 2013
 http://nyumbayahabari.blogspot.com

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.