Thursday, May 2, 2013

MADAWA YA KULEVYA YATAJWA KUSABABISHA KIFO CHA MEMBER WA KRISS KROSS / Chris Kelly

Kwa mujibu wa ripoti ya polisi Kriss Kross Rapper Chris Kelly alikua anatumia madawa ya kulevya aina ya cocaine na heroin muda mfupi kabla ya kifo chake.
Inasemekana kwamba gari la wagonjwa huku likiwa na wataalam wa afya lilifika nyumbani kwa kina msanii baada ya mama wa chriss kupiga simu, na alikutwa amelala kwenye kochi huku kukiwa hakuna dalili za uhai, mwili wake ukabebwa fasta kuelekea hospitali ya karibu, na masaa machache baadae akatangazwa ameaga dunia.

Baada ya kifo, polisi walifanya mahojiano na mama mzazi wa CHRIS na aliwaambia polisi kwamba usiku mmoja kabla ya mtoto wake kuzidiwa alikua ametumia mchanganyiko wa madawa ya kulevya ya heroin na cocaine, ambao unajulikana kama SPEEDBALLS.

Mama huyo akaongeza kuwa binafs aliamua kumrudisha mwanae nyumbani ili aweze kuacha kutumia madawa ya kulevya kama alivyowahi kufanya siku za nyuma, na asubuhi yake alikua anaumwa tumbo / nauseous
Masaa kadhaa kabla ya kifo cha member wa kundi la kriss kross alifanya interview na The Streetz Morning Grind radio show na alikua ana sound kama mtu flani ambaye hayuko sawa kiafya.
Skiza simu hiyo hapo chini:


MUSIC VIDEO ILIYOWAPA UMAARUFU KUNDI LA KRISS KROSS 

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.