Wednesday, May 15, 2013

NIKKI WA PILI : WARAKA WA WEUSI KAMPUNI KWA WA TANZANIA KUHUSU MLIPUKO WA BOMU NDANI YA KANISA ARUSHA

                                                     
member wa WEUSI KAMPUNI kutoka kushoto ni Joh Makini, Nikki Pili na G Nako
Kufuatia mlipuko wa bomu uliotokea tarehe 4 mwezi wa tano katika kanisa la kikatoliki huko olasisti nakupelekea vifo na majeruhi kwa baadhi ya waumini waliohudhuria katika sherehe ya ufunguzi wa kanisa hilo, zikawepo rumors kuwa eti mlipuko huo unahusiana na tofauti za kidini, sasa weusi kampuni, inayoundwa na baadhi ya wasanii wenye nguvu kutoka arusha, hapo nawazungumzia kina joh makini, g nako, bonta, lord eyez, na nikki wa pili wametoa waraka.

Usome hapo chini

Nafahamika kama Nicksson Simon ama Niki wa Pili mzawa na nimekulia Arusha, kuhusiana na suala ambalo limetokea Arusha kwanza kama Weusi Kampuni / wakazi Arusha tunatoa pole sana kwa watu ambao wameathirika na hilo janga, wale ambao wamepoteza maisha mungu awalaze mahali pema peponi, na wamepoteza maisha katika harakati ya kutetea uhuru wao na nchi yao.
Sisi Tamko letu ni kwamba WEUSI tumeliangalia hili suala kwa kina na tumegundua yafuatayo:-
  1. Tanzania hakuna udini, kwa sababu watanzania wote tumesoma shule moja, tunaishi pamoja tunashirikiana, tunaowana, tunashiriki maulidi, wakristo tushaalikwa futari so tunakula futari, tunashiriki harusi tunashiriki harusi tunashiriki sherehe.  
kwa hiyo hakuna mtanzania mmoja mmoja aliyewahi kukumbana na kasumba ya kidini au kubaguliwa kidini au kutengwa kidini, kwa hiyo Udini Tanzania hakuna, sasa kama udini hakuna tatizo ni nini?
Ili kuweza kuelewa hili tatizo vizuri tuangalie na ulimwengu sasa hivi uko wapi? umetoka wapi na nini kinaendelea.

Moja kati ya majeruhi wa bomu la Arusha
Dunia sasa hivi katika muanguko wa kiuchumi, crisis ya dunia inayofata ni energy kwa kiswahili ni Nishati yani gesi, mafuta pamoja na madini, sasa basi historia inatuambiaje katika zile nchi ambazo zimekua na hizi rasilimali Africa pande nyingine za dunia, tuangalie congo kuna madini Nigeria kuna Mafuta, Sudan kuna mafuta, somalia, iraq, libya, syria, na kule south america Venezuela kote kuna mafuta, ni hivi sasa ili ubepari uweze kupata hizo rasilimali katika nchi flani eneo lolote duniani Theory yao mbayo wanaitumia tangu zamani mpaka sasa hivi, zile nchi inabidi zichafuliwe ziwe nchi za machafuko ili serikali ishindwe kusimamia rasilimali zake, sasa wakati machafuko yanaendelea wao wanafanya uvunaji wa hizo rasilimali,

tunaona uvunaji unaendelea Nigeria, Congo, Sudan, mpaka sasa hivi takwimu zinaonyesha wa Congo milioni 5 washapoteza maisha, wa Sudan takriban watu laki 3 washapoteza maisha, hili tukio linatokea Tanzania leo hii kwa sababu leo hii Tanzania kuna uvumbuzi mkubwa umetokea kuna Uranium, gesi na mafuta kwa hiyo Theory ni ile ile kama ilivyofanyika nchi nyingine inaletwa Tanzania, sasa tunaletewa Adui wa bandia, haya machafuko yanaweza kuja kwa picha nyingi, unaweza ukaletewa kwa picha ya Udini, harakati, maandamano, watu wanakaa ni wasomi inaitwa conspiracy Theaory,

watu wasomi wanakuja katika nyanja mbalimbali lakini lengo ni kuchukua rasilimali na kutengeneza vita au machafuko katika eneo ambalo rasilimali zinapatikana, kwa hiyo watanzania wanatakiwa waelewe kitu kimoja tu huu udini unaosemwa ni adui wa bandia anatengenezwa, kinachotakikana haswa ama tatizo ni rasilimali zinatakiwa zichukuliwe na nchi kama Tanzania inaonekana kwamba ukiruhusu ikatumia rasilimali zake vizuri ndani ya miaka 20 au 25 inaweza ikawa kama........................................
MALIZIA KUSKIZA WARAKA HUU KWA KUSKIZA SAUTI HIYO HAPO CHINI:


Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.