Monday, May 19, 2014

YOU HEARD: MRISHO MPOTO KUTOA DONGE NONO KWA ATAKAYEWEZESHA KURUDISHA PAGE YAKE YA FACEBOOK

Kufuatia Mzee mmoja kujitokeza na familia yake na kudai kuwa eti ametapeliwa kwa njia ya mtandao na msanii Mrisho Mpoto, yeye mwenyewe amejibu kuwa kwa siku tatu zilizopita ameibiwa page yake ya facebook yenye watu zaidi ya elfu 50, sasa aliyeiba page hiyo ndo anawatapeli watu kwa kujidai eti kuna mkopo unatolewa na taasisi ya Vicoba, na mpaka leo Mpoto hawezi kufanya lolote kwenye page hiyo, yani si yake tena, Hali hiyo imesababisha msanii kuahidi donge nono la milioni moja kwa mtu atakayewezesha kurudisha page hiyo.
Maharamia hao wamepost kwenye page ya www.facebook.com/mrishompoto

HABARI MUHIMU KWA WATANZANIA WOTE.
#BREAKING_NEWS:
Taasisi ya Vicoba Tanzania imezindua rasmi mtandao / tovuti http://focus-vicoba.wapka.mobi/ kupitia mfuko wa utoaji mikopo kwa watanzania wote uitwao FOCUS VICOBA ili kurahisisha upatikanaji mikopo kwa haraka kwa watanzania na kumuwezesha kila mtanzania kujiunga vicoba na kupatiwa mkopo popote pale alipo kwa urahisi zaidi. Mtanzania ataweza kutembelea tovuti yao http://focus-vicoba.wapka.mobi/ na akajiunga kwa kujaza fomu zao na kuweka akiba zake na kupatiwa mkopo. Ni rahisi, salama na haraka.

Riba nafuu pia zawadi za bajaji na boda boda zinatolewa kwa watakao chukua mkopo mkubwa ili kusaidia marejesho. Hii ni fursa kwa kila mtanzania kuweza kujiunga na kupatiwa mkopo.

#UJUMBE: "Nipo studio na Banana Zorro tunatengeneza wimbo kwa ajili ya matangazo ya Vicoba na video itatengenezwa hapo kesho, siku ya jumatatu itakua hewani katika media mbali mbali"


Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.