Monday, June 9, 2014

YOU HEARD: ALAWI JUNIOR APOKONYWA GARI ALILOPEWA KAMA ZAWADI

Lile gari aina ya Lexus ambalo msanii wa bongo flava Alawi Jr alitangaza kuwa amepewa zawadi na shabiki wa muziki wake inasemekana kuwa Shabiki huyo wa Alawi Jr ameamua kuuchukua usafiri wake na kumwacha msanii huyo asijue la kufanya kwasababu tendo hilo hakua analitegemea, Snitch wetu ametuhabarisha kuwa eti Alawi Jr kwa wakati huu imebidi ajiibie kwenye usafiri wa bajaj au mara nyingine inabidi aombe lifti au akodi Taxi, alipopigiwa simu na Gazeti la Makorokocho kuulizwa juu ya mkasa huu Alawi alikanusha Taarifa hizi na kudai kuwa Gari hilo limeharibika na amelipeleka Garage maeneo ya Kinondoni wala hana haraka nalo, alipoulizwa kama mara ya kwanza alipewa na kadi ya Gari Alawi aliskip kwa mbaaaali, juhudi za kumpata Mwenye Gari hilo anayefahamika kwa jina la Tom au Baba Maya zinaendelea kwani tumeambiwa ameelekea Brazil kwa ajili ya fainaliza za kombe la dunia Brazuuuuka.

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.