Wednesday, August 31, 2016

Chris Brown atozwa kiasi cha $250,000 kama dhamana dhidi ya tuhuma za kumtisha mtu na silaha.

 

Licha ya kusuburiwa kwa muda mrefu na polisi kwenye nyumba yake usiku wa kuamkia August 31 huko Las Angeles na hatimae kukamatwa na polsi ikiwa ni  baada ya mwanamke aliedai kuwa Mwanamuziki Chris Brown alimtishia na silaha nzito,hatimae Mwanamuziki huyo ameachiwa kwa dhamana ya $250,000.Hata hivyo ni bahati mbaya kwa Chris Brown kwani licha ya kuwa historia ya makosa ya jinai,polisi wamedai kuwa wakati wa upekuzi kwenye nyumba yake walikuta begi lenye madawa ya kulevya na silaha.



 

Chris Brown,aliekaa chini mwenye kofia nyekundu.


  Mara baada ya kupata Dhamana hiyo Mwanasheria wa msanii  huyo Mark Geragos  amedai  kuwa mteja wake yupo salama na kudai kuwa tuhuma za Baylee Curran mwanamke anaedai kuwa Breezy alimtishia na silaha barabarani kama  ilivyoripotiwa na mtandao wa  TMZ hazina ukweli wowote  kwani Mwanamke huyo ana historia ya kuhusihwa na matukio ya fujo ambapo inadaiwa kuwa mnamo mwaka 2013 Mwanamke huyo akiwa na marafiki zake au kibongo tuseme na mashosti zake kwenye     mgaahawa wa Pizza aliwatoroka wenzake akiwa na mkoba aina ya Louis Vuitton huku mkoba huo ukiwa na kiasi cha $200,Kadi za benki na nyaraka nyingine hivyo licha ya madai yake dhidi Brezy, Polisi wamedai kuwa Mwanamke huyo alikua akisakwa na
maafisa wa NYPD.

 
Byleen Curran. 

 

Chris Brron ataendelea kupunga upepo uraiani akisubiri kuripoti tena Mahakamani  tarehe ishirini ya mwezi September.

Kama kawa Team Makarokocho tutanyapia kitakachojiri na kuwa-uptodate.

Chris Brown.

 

 

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.