Thursday, September 1, 2016

Baada ya Prf.Lipumba kulia,Ofisi ya msajili wa vyama yamlima barua Maalim Seif.

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya siasa nchini imemuandikia barua Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad kufuatia mvutano wa kusimamishwa uanachama aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba.


Hatua hiyo imefikiwa baada ya Profesa Lipumba kumuandikia barua Msajili wa vyama vya siasa nchini, Jaji Francis Mutungi akilalamikia kusimamishwa uanachama bila kufuata utaratibu huku akitaka kurejeshwa kwenye nafasi yake ya uenyekiti.

     Aliekua Mkt.wa Chama cha C.U.F,Prof.Ibrahim Haruna Lipumba.

Ofisi hiyo imeutaka uongozi wa CUF kueleza kwa kina hatua ilizopitiwa hadi kufikia uamuzi huo kwa mujibu wa katiba ya chama hicho, na kwamba chama hicho kiwasilishe majibu  kwa barua barua Sept.2.

Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano cha Ofisi ya Msajili wa Vyama Vya Siasa, Monica Laurent amesema kuwa ofisi hiyo ilipokea barua ya Profesa Lipumba Agosti 29 mwaka huu ikiwa na malalamiko na kwamba wametaka uongozi wa CUF kutolea majibu.

“Tumeitaka CUF kutoa majibu kuhusu malalamiko ya Profesa Lipumba, ndipo sisi tutakapotoa majibu,” amesema Monica.

        Katibu mkuu wa Chama cha C.U.F,Maalim Seif Sharif Hamad.

Lipumba ambaye alijiuzulu nafasi yake ya Uenyekiti mwaka jana akipinga uamuzi wa chama chake kumuunga mkono Edward Lowassa kugombea urais, amerejea na kudai kutengua barua yake ya kujiuzulu.

Baraza Kuu la CUF lililoketi visiwani Zanzibar hivi karibuni lilimsimamisha uanachama Profesa Lipumba pamoja na viongozi wengine 10 akiwemo Mbunge wa Kaliua, Magdalena Sakaya aliyekuwa Naibu Katibu mkuu (Bara).

Hata hivyo, Profesa Lipumba amepinga uamuzi huo akieleza kuwa kikao cha baraza hilo kililiwa batili. 


#UbuyuMtamuWaShilawadu...Doh.
 

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.