Vijana wanaojihusisha na biashara ya usafirishaji kwa kutumia
usafiri wa pikipiki maarufu kama bodaboda, asubuhi ya leo (jumanne)
wamejitokeza kwa wingi katika hoteli aliyofikia waziri mkuu huyo mstaafu
na mjumbe wa kamati kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo,CHADEMA.
Katika malalamiko yao vijana hao wamelalamikia ugumu wa maisha hasa
mfumuko wa bei katika mkoa huo, kukosekana kwa pesa kwenye mzunguko na
hali ngumu ya maisha kwa ujumla katika kipindi hiki cha kuelekea sikukuu
za mwisho wa mwaka.
Vijana hao pia wamemlalamikia Mh. Lowassa kuhusu kunyang'anywa vyombo
vyao vya kufanyia kazi na waajiri wao kutokana na kutofautiana itikadi
za kisiasa.
Chanzo:Mashuhuda wa SHILAWADU,Tabora.