Saturday, April 7, 2012

KIFO CHA KANUMBA NI CHA KUPANGWA NA WATU FLANI FLANI, AU NATURAL? MWANAUME ALIYEKAMATWA NA LULU, KABLA HAWAJAKUTANA ALIKUA MOCHWARI NA KINA RAY WANAOMBOLEZA, ALIKUA ANAJUA FIKA KUWA LULU ANATAFUTWA NA POLISI, SWALI JE KWANINI HAKUTOA TAARIFA POLISI?


                                     R.I.P Steven Charles Kanumba (8/01/1984- 7/04/2012)
TUKIO LILIVYOKUA JANA USIKU:
Mida ya Saa Sita usiku, Steven Kanumba akiwa na Mpenzi wake wa siri (LULU) alitoka Chumbani na kwenda kuoga ili aingie viwanja, alipomaliza wakati anarudi chumbani akamskia mpenzi wake kwa mbali anaongea na simu, kufungua mlango akamuuliza unaongea na nani mida hii? Akajibiwa kuwa kuna Kampuni inataka kumpa deal ya Movie, lakini yeye Kanumba katika hali ya kawaida akaona haiwezekani saa sita za ucku watu wapeane deal, wakaanza kujibizana, huku Kanumba akimshushia Kichapo Lulu, ndipo huku na huku mwanadada akaona ajitetee, mwisho wa siku Kanumba akasukumwa na kuangukia kisogo na kuwa Kiiiiiimya, Lulu ndo akashtuka na kwenda kumwita mdogo wake Kanumba ambaye alikua chumba kingine, dogo kufika na kuona hali ya Bro, ikabidi atoke Nje kufanya ustaarabu wa kumtafuta Daktari ili aje kuokoa maisha ya Kanumba na vile vile kuwashtua ndugu na jamaa, ndipo Lulu akapagawa na kupata upenyo wa kutoroka eneo la Tukio, watu kufika Kanumba alishakuwa wa baridi cku nyiiiiingi, ikabidi utaratibu wa kuupeleka mwili wa marehemu hospitali ya Taifa Muhimbili ukafanyika.

BAADA YA MWILI WA KANUMBA KUPELEKWA MOCHWARI:
Saa nane za usiku, ndipo baadhi ya wasanii wakaanza kujadili yuko wapi aliyesababisha Kifo hicho? (LULU) wakatoa taarifa polisi sasa kumbe kuna kijana anaitwa Junior miongoni mwa kundi hilo, akaziskia taarifa hizo, na baada ya muda mfupi kwa siri akampigia simu Lulu kuwa wakutane mahali, anataka ampatie mkanda mzima, basi wakapanga na kukutana maeneo flani kwa siri.

                           Actress: Lulu Michael Mtuhumiwa namba moja wa Kifo cha Kanumba
LULU ALIVYOKAMATWA:  
Inasemekana Polisi walifanikiwa kuwakuta kwa pamoja, ndipo waigizaji wakashtuka, Duh!! Huyu si tulikua naye huyu?
Lulu alikutwa akiwa naked(bila Nguo) huku akiwa amepagawa, Yes of coz lazma awe amepagawa katika hali kama hiyo, lakini pia alikutwa ameumizwa vibaya usoni, (hiyo ina maana kuwa walipigana na Kanumba)
Sijataja mahali walipokutwa na baadhi ya majina kwa sababu za kiusalama, coz bado upelelezi wa polisi haujakamilika.

KUTOKANA NA KOSA LA KUUA BILA KUKUSUDIA, LULU KUHUKUMIWA ZAIDI YA MIAKA MIWILI JELA:
Endapo muigizaji wa Kike Lulu Michael atakutwa na hatia pindi atakapo pelekwa mahakamani basi huenda akahumiwa kuanzia miaka miwili na kuendelea, kama ilivyotokea kwa Daktari wa Michael Jackson (Dr Conrad Murray) nchini marekani,
Ila kesi yake inaweza kuwa ndefu zaidi kutokana na yeye Lulu kutoroka eneo la tukio muda mfupi tu baada ya Kanumba kufa.

IMEANDIKWA NA MSOMAJI WA BLOG JINA KAPUNI

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.