Tuesday, May 27, 2014

RACHEL HAULE WA BONGO MOVIE KUZIKWA SONGEA



Sekta ya bongo movie  imepoteza jembe lingine rachel haule, aliyefariki leo asubuhi kutokana complication zilizotokea jana usiku baada ya kujifungua kwa operation , mtoto akafariki na rachel akalazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi,  ilipofika asubuhi ya leo Rachel Haule akaaga dunia.
Amewahi kucheza filamu nyingi  kama: Siku za majaribu, mtihani, na movie za odama chini ya Kampuni J film for life,  na filamu ya hivi karibuni kucheza ilikua Vanesa in Dillema.
Leo asubuhi wasanii wa bongo walikutana pale Leaders club pamoja na maelezo kutoka kwa ndugu wa marehemu ikaamuliwa kuwa mwili wa Recho Haule utasafirishwa kwa ajili ya maziko pamoja na mwili wa mtoto wake mchanga aliyefariki kuelekea Songea ambako kuna bibi yake pamoja na mtoto wake mkubwa, wazazi wa Recho Haule walifariki siku nyingi.

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.