Saturday, May 10, 2014

YOU HEARD: WAKATI MASTER JAY ANAJIPANGA KUMTANGAZA SHAA KAMA MCHUMBA WAKE, MKE WAKE WA NDOA NAE KUMTANGAZA SERENGETI BOY WAKE

Shaa na Master Jay
Wakati tetesi mtaani zinadai Producer mkongwe Master Jay ana mpango wa kuandaa mkutano wa waandishi wa habari ili kumtambulisha Mwanadada Shaa kama mchumba wake, ikiwa ni ya baada ya MJ kushawishiwa na mama yake mzazi ambaye anafahamu mahusiano ya wawili hao kwa karibu miaka 10 au zaidi, sasa Gazeti la makorokocho limetonywa juu ya Serengeti boy aliyemrithi MJ kwa Wife wake Rose Marry,
Bibie Rose Marry

Kwanza kabla sijakuambia kuhusu Serengeti boy K Style, ngoja nikuambie situation iliyopo kati ya Master Jay, RoseMarry (Wife wake MJ waliyefunga ndoa ya kanisa) na Shaa, zaidi ya miaka 10 iliyopita Mj na RoseMarry mahusiano yao yalianza kulega lakini kutokana na ndoa ya Kanisani haivunjiki kirahisi ikabidi watengane nyumba,  Mj akaanzisha mahusiano na msanii Shaa, Mj akahamia katika nyumba yake nyingine Mbezi pamoja na Shaa na kumwacha bibie Rose pamoja na watoto wao watatu waishi Masaki pale ambapo zipo studio za MJ Records ambapo wanaishi mpaka leo na ndoa hiyo imeshindikana kuvunjika na hawashirikiani kinyumba, back to the point Serengeti boy wa Rose Marry namwita serengeti boy kwasababu umri wake ni mdogo, ingawa wataalamu wa mambo wanasema age is nothing but a number, sasa inasemekana eti Mrithi wa Mj ni msanii wa Bongo Flava mwenye swagg nyingi anapo Rap na ni mshindi wa shindano la Serengeti Fiesta 2013 KStyle na wao wanampango wa kujitangaza rasmi, Nilipomuliza Master Jay kuhusu msanii huyo kumrithi akanijibu "ni vyema unajua tena binadamu tunatakiwa kuwa wawili wawili"
Huyu ndo Mrithi wa Mj Rapper K Style
Skiza You Heard hapo chini kama ilivyokua jana kwenye XXL ya Clouds fm



Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.