Monday, August 4, 2014

YOU HEARD: WIMBO WA GERE WA WEUSI NI COPY YA PESO YA MACHINE GUN KELLY?

Taarifa zilizohit kwenye mtandao wa Makorokocho zinadai kuwa eti Wimbo wa Kundi la Weusi unaitwa "Gere" eti Mdundo wake ni Copy ya wimbo wa Msanii wa HipHop kutoka Cleveland Marekani anayeitwa Machine Gun Kelly na wimbo wake unaitwa Peso amewashirikisha Ma rapa Meek Mill na Pusha T uliotoka mwanzoni mwa mwaka 2013, akizungumzia Ishu Hii Rapper Joh Makini amekanusha na kupiga pasi kwa Mtaarishaji wa wimbo wa Gere Producer Nahreel kwa sababu yeye ndiye aliyehusika kwenye Upishi wa ngoma nzima, kwani wao waliikuta beat imeshatengenezwa.
Producer huyo alipovutiwa Wire na Gossip Cop Tz aliruka futi mia na kudai kuwa tuhuma hizo si za kweli kwasababu kama yeye angekua anatabia mbaya za ku copy midundo ya watu basi ingejulikana siku nyingi.
Wimbo wa Gere Umetoka mwishoni mwa Mwaka jana na kufanya vizuri kwenye chart za radio mbalimbali sambamba na video ya ngoma hii pia imefanya vizuri pia.
Machine Gun Kelly
Producer NahReel wa Switch Records
SKIZA WALICHOONGEA KUPITIA YOU HEARD YA XXL CLOUDS FM

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.