Sunday, September 11, 2016

PICHA:Gari la matairi 3 inayotumia umeme badala ya mafuta.

Gari mpya imeingia sokoni kwa dola za Kimarekani 15,000, na imekuja na muonekano tofauti kabisa na gari nyingine unazozifahamu. Yenyewe inatumia umeme na inatumia matairi matatu kama bajaji lakini inatumika na mtu mmoja pekee.

Gari hii imetengenezwa na Kampuni kutoka Canada, inayofahamika kama kama Electra Meccanica. ambapo  itaanza  kuwa barabarani ifikapo mwaka 2017.Gari hili  limepewa jina SOLO kutokana na kuwa na uwezo wa kubeba mtu mmoja tu.
Imetengenezwa sio kwa lengo la kukuhamisha wewe kutoka katika kutumia gari nyingine,bali kukurahisishia mizunguko yako ya hapa na pale.

Inauwezo wa kutembea kwa spidi ya maili 80 kwa saa,Ikiwa na  betri ya yenye madini aina ya lithiam inayojichaji kila baada ya umbali wa maili 100. 100.Muda unaotumia kuchaji gari hiyo unategemea na uwezo wa chaji yako ( voltage). 220V utakaa mpaka masaa 3 kuicharge, na kwa 110V itakaa mpaka masaa sita ikiwa kwenye chaji.

Tazama picha tofauti za gari hilo ; 



Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.