Monday, September 12, 2016

Young Thug Amevunja Rekodi Ya Billboard Pia Afungukia Uvaaji Wake Wa Nguo Za Kike.




Mixtape yake aliyoipa jina la “Jeffery” ambayo iliingizwa rasmi sokoni tarehe 25, 08 mwaka huu imemfanya Young Thug Kuvunja recodi ya Billboard kwa kuingiza rekodi ya kushika nafasi za juu kwa albamu tatu tofauti kwenye chati mbalimbali.


“Jefferry”ambayo  iliingia kama namba nane kwenye Billboard Top 200 imetajwa kuuza kopi 37,000 ndani ya wiki yake ya kwanza.


Mapema mwezi Februari mnyamwezi Young Thug  aliachia Mixtape "I'm Up" ambayo iko nafasi ya sita, iliuza kopi 15,000 kwenye wiki yake ya kwanza iliyofuatiwa na  "Slime Season 3" ambayo nayo kwenye wiki yake ya kwanza iliuza kopi 22,000.


Artwork  ya mixtape Jaffery ambayo inamuonyesha mtu mzima Young Thug akiwa amevaa gauni ni stori kubwa amabayo iliwafanya watu wengi kuwa na maswali mengi kwa Young Thug huku wengine wakidai ameharibikiwa

 “Linapokuja suala la swagga hatujali jinsia gani wanapendeza mavazi gani” aliswahi kuongea Young Thug kwenye moja ya Interview zake. “Nikiliona lile gauni huwa nahisi ni kama Mungu ndie alinipatia” aliongeza Young Thug.
Young Thug pia alikiri kuanza kuvaa nguo za kike tangu akiwa na umri mdogo na hajawahi kuwa na matatizo yeyote ya kijinsia.
“Nilipokua na miaka 12 miguu yangu ilikua midogo sana hivyo nilikua napenda kuvaa viatu vya dada zangu” Ilifika hatua baba yangu alikua anakasirika kiasi cha kunizuia kutoka kokote kwa kudai nitamuaibisha lakini mimi sikuwa naikijali watu wataongea nini”

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.