Thursday, October 6, 2016

Simu ya Sumsung yawaka moto ndani ya ndege.

Simu ya kampuni ya Samsung aina ya Galaxy Note 7, ambayo awali ilithibitiishwa na kampuni hiyo kuwa ilikuwa salama, imezua taharuki baada ya kushika moto kwenye ndege nchini Marekani.

 Simu hiyo ilirushwa kwenye sakafu, mmiliki wake Brian Green amesema

Simu hiyo inadaiwa kushika moto ikiwa mikononi mwa abiria aliyekuwa kwenye shirika la ndege la Southwest Airlines.Shirika hilo limesema abiria waliokuwa kwenye ndege yao iliyokuwa imepangiwa kusafiri kutoka Louisville, Kentucky, hadi Baltimore, Maryland, waliondolewa kwenye ndege kwa dharura kabla ya ndege hiyo kupaa Jumatano kutokana na kisa hicho cha simu kuwaka moto.

Kampuni ya Samsung iliwashauri watu waliokuwa wamenunua simu za Note 7 kuzirejesha kwa kampuni hiyo baada ya kugunduliwa zilikuwa na tatizo kwenye betri zake ambapo Samsung imesema bado inachunguza kisa hicho cha Jumatano.
 Samsung Note 7

 Mmiliki wa simu hiyo Brian Green, akizungumza na Jordan Golson wa shirika la The Verge, amesema alinunua simu hiyo tarehe 21 hii ikiwa ni baada ya Sumsung kuzirudisha sokoni simu mpya za Sumsung Gulaxy Note 7 ikiwa na alama ya mraba ya rangi nyeusi kwenye pakiti yake, alama ambayo iliongezwa na Samsung kutofautisha kati ya simu zilizokuwa zimeuzwa awali ambazo zilidaiwa kutokuwa salama na kuongeza kuwa,Mara baada ya simu hiyo kushika moto aliitupa nnje kupitia dirishani.

 "Abiria mmoja alitufahamisha kuhusu moto uliokuwa unafuka kutoka kwa simu. Abiria wote na wahudumu wa ndege waliondolewa salama kutoka kwenye ndege." .Msemaji wa Shirika la ndege la Southwest Airlines aliiambia BBC.



Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.