Thursday, October 6, 2016

VIDEO:Taarifa rasmi kuhusu walimu 3 waliomshambulia mwanafunzi kwa kipigo Mbeya na adhabu waliyopewa.




Kwa mujibu wa Waziri wa mambo ya ndani ya Nchi,Mwigulu Lameck Nchemba ambae alilifatilia kwa karibu sakata hilo ameeleza kuwa  mnamo tarehe 28.9.2016 mwanafunzi aitwae Sebastian Singuli wa kidato cha 3A katika shule ya kutwa ya mbeya wilayani uyole alipigwa na walimu watatu,Mwl.Frank msigwa,John Deo (UDSM) na Sanke Gwamaka (Mwl.Nyerere Memorial) wote  wakiwa shuleni hapo kwa ajili ya mafunzo ya vitendo (field).


Inadaiwa kuwa Mwl.Frank Msigwa alitoa zoezi la somo la kingereza na baadhi ya wanafunzi hawakufanya akiwemo Sebastian.Akiwa darasani mwalimu huyo alimpiga kofi Sebastian ndipo akamhoji kwanini anampiga kabla kukabana na koo na hatimae mwalimu huyo akishirikiana na wenzake walimpeleka ofisini na kuanza kumpiga huku mwalimu aliefahamika kwa jina Ester Harembo kutoka Chuo Kikuu Iringa akiwasihi waache kumshambulia mwanafunzi huyo kwa kipigo bila mafanikio.

Hata hivyo tangu tarehe 29 Septemba mwanafunzi huyo hakuonekana shuleni kutokana na majeraha ambapo walimu hao hawapo tena shuleni hapo kutokana na muda wao wa mafunzo ya vitendo kumalizika.

Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya linamshikilia Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo kwa mahojiano ambapo Waziri Nchemba amegiza kukamatwa kwa walimu hao,huku Waziri wa Elimu,Sayansi na Mafunzo ya Ufundi Prof.Joyce Ndalichako amewafukuza chuo walimu hao na kudai kuwa kwa mujibu wa taratibu za vyuo vikuu walimu hao wametenda kosa la jinai na hawawezi kuendelea na kazi ya ualimu kwakua wamekosa sifa za taaluma hiyo na kuongeza kuwa kitendo kilichofanywa na walimu hao sio cha kufumbiwa macho na jamii.

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.