Kwa mara ya kwanza katika historia ya mabenki ukiacha enzi zile za Meridian Biao, ni wazi sekta ya benki nchini inapitia hali tete hii ikiwa ni baada ya benki kongwe ya Barclays tawi la Tanzania kutoa taadhari kwa wafanyakazi wao kwamba benki yao inapitia kipindi kigumu kifedha hivyo kuamua kufuta baadhi ya shughuli ndogo kabisa kama sherehe za 'Family Day'.
Taarifa imekuja baada ya benki ya CRDB nayo kutoa mchanganuo uliobaini hasara ya bilioni kwenye .hesabu zake za robo mwaka (Quarterly Financial Statements).