Sunday, December 11, 2016

Antony Lusekeleo 'Mzee wa Upako',awaombea kifo waandishi wa habari,kisa..!?

Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) lililopo Ubungo Riverside jijini Dar es salaam, Anthony Lusekelo, maarufu kama Mzee wa Upako amesema waandishi wote wanaoandika habari za kumchafua watakufa kabla ya kufika Machi mwakani.

Kauli hiyo aliitoa kwenye ibada ya Jumapili ya tarehe 11 ya mwezi Disemba 2016,ikiwa ni mwendelezo wa mahubiri yake ya nne katika wiki ya tatu mfululizo, akijibu yaliyoandikwa kwenye vyombo vya habari kuhusu kumfanyia fujo jirani yake,huku akidaiwa kufanya kitendo hicho akiwa amelewa.

“Kila mwandishi aliyeniandika vibaya ikifika mwezi wa tatu akiwa hai, mimi naacha kuhubiri, nafunga virago nakwenda kuuza gongo, sasa Mungu ndiye ataamua kwamba ama niache kuhubiri mimi au wewe ufe …najua hata leo mpo humu mmekuja na mnasikiliza tu,” alisema. 

Chanzo:Mwananchi.

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.