|  | 
| Hammer Q | 
|  | 
| Bibie Salha baada ya kuchezea kichapo | 
Msanii maarufu wa muziki wa taarab Hussein Mohammed a.k.a Hammer Q jana
 amempa kipigo cha mbwa mwizi mkewe Bi Salha Abdallah kwa tuhuma za 
kudaiwa talaka na mkewe huyu ili aende kwa kijana ambaye yeye alikuwa 
akimtamka kwa jina la Sharo baro, Mtuhumiwa huyo ambaye ndiye 
anayesadikiwa kuwa chanzo cha ugomvi huo wa wanandoa hao ni Mtoto wa 
Moshi william ambaye anajulikana kwa jina la Hassan Moshi. 
Tukio hilo lilianzia Dar Live 
ambapo kulikuwa na uzinduzi wa Bendi ya 5 star, inasadikiwa Mtoto wa 
Marehemu TX Moshi William alikuwa akisalimiana na Mke wa Hammer Q na mke
 wa Hammer Q akamuomba mumewe amtambulishe kwa Rafiki yake huyo (Hassan 
Moshi), baada ya kumtambulisha ugomvi ndio ukaanzia hapo. Watonyaji wa 
habari hiyo wakasema Hammer Q alianza kumpa kichapo mkewe huyo ambaye 
alikuwa yupo kwenye maandalizi ya sherehe ya kitchen Party yake ambayo 
ilikuwa ifanyike Tarehe 24/05/2013 ingawa harusi ilikuwa tayari 
imeshafanyika. 
Baada ya Songombingo hilo 
kutulizwa na washkaji zake Hammer Q wanandoa hao wakatulia, wakashiriki 
shughuli hiyo ya uzinduzi mpaka ilipoisha na baada ya hapo wakaondoka na
 kuanza safari ya kuelekea nyumbani kwao Magomeni ambako pia wana mji 
wao ukiachilia kule kigamboni. Kwa mujibu wa Hammer Q anasema alipofika 
nyumbani mkewe huyo alianza kumsemea maneno ya kashfa na kuanza kumdai 
talaka na ndio hasira zikampanda na kuanza kumpelekea kipigo cha MBWA 
MWIZI kwa mujibu wa majirani walioshuhudia tukio hilo, Hammer Q 
aliendelea kumpiga mkewe huyo kama vile anataka kumtoa Roho, majirani 
walipokuwa wanaingilia ili kuweza kusuluhisha inasadikiwa Hammer Q akawa
 anasema anampiga mkewe huyo kwa sababu amemuoa na amemgaramia, tukio 
hilo la kikatili lilidumu takribani nusu saa mpaka pale wasamaria wema 
walipofanikiwa kumnasua mkewe huyo katika mikono ya mumewe huyo (Hammer 
Q) ambaye wadau wengi wanasema ni mchezo wake kuwapa vichapo wale ambao 
huwa na mahusiano nao kimapenzi kwa kisingizio cha wivu. 
Hata hivyo baada ya tukio hilo
 wasamaria wema walimpeleka Salha (Mke) mpaka hospitali ya magomeni kwa 
matibabu na kwenda kufungua kesi katika Kituo cha polisi cha magomeni, 
Wafuatiliaji wetu hawakuishia hapo ikawalazimu wampigie simu Hammer Q 
kutaka kujua zaidi ana uamuzi gani kutokana na kitendo chake hicho 
lakini yeye alikiri kufanya kitendo hicho cha kikatili na kuishia 
kuwaomba samahani watanzania, wanafamilia ya Mkewe huyo pamoja na 
majirani kwa kusema haikuwa dhamira yake ila ni POMBE tu ndio 
zilimpelekea afanye kitendo kile.
Familia ya Baba yake Salha 
(Mke) wametaka Hammer Q akamatwe haraka sana kwa kutenda kitendo cha 
kikatili ambacho hakikubaliki kwenye jamii ya Watanzania wa karne hii, 
pia kwa mujibu wa Mke (Salha) amesema Hammer Q alishamwandikia talaka 
yake kwa maelezo ya talaka tatu ambayo alikata kijikaratasi kimoja na 
kumwandikia kama talaka, Wadau mtatusaidia kama talaka hiyo ni halali au
 La! 
Taarifa zaidi tutawaletea kama
 ameshakamatwa au La! ingawa majirani wanasema walipokuwa wanampigia 
simu alikuwa anasema anataka kujiua kwa kudhani yeye alishakuwa amemuua 
Salha (Mke) kwa sababu alipokuwa anatolewa nyumbani alikuwa amezimia hajitambui. Salha ameshonwa nyuzi kadhaa kichwani na mkononi.
wakati akihojiwa na GEAH HABIB wa leo tena ya clouds fm, Hammer Q amesema ni shetani tu alimpitia
Story kwa hisani ya
kapingaz.blogspot.com
Story kwa hisani ya
kapingaz.blogspot.com
 
 
 
 
