Wednesday, May 1, 2013

MSANII WA BONGO HAMMER Q AMPIGA MKEWE KIPIGO CHA MBWA MWIZI: AZIMIA MASAA KADHAA, ASHONWA NYUZI KADHAA


Hammer Q

Bibie Salha baada ya kuchezea kichapo 


Msanii maarufu wa muziki wa taarab Hussein Mohammed a.k.a Hammer Q jana amempa kipigo cha mbwa mwizi mkewe Bi Salha Abdallah kwa tuhuma za kudaiwa talaka na mkewe huyu ili aende kwa kijana ambaye yeye alikuwa akimtamka kwa jina la Sharo baro, Mtuhumiwa huyo ambaye ndiye anayesadikiwa kuwa chanzo cha ugomvi huo wa wanandoa hao ni Mtoto wa Moshi william ambaye anajulikana kwa jina la Hassan Moshi.
Tukio hilo lilianzia Dar Live ambapo kulikuwa na uzinduzi wa Bendi ya 5 star, inasadikiwa Mtoto wa Marehemu TX Moshi William alikuwa akisalimiana na Mke wa Hammer Q na mke wa Hammer Q akamuomba mumewe amtambulishe kwa Rafiki yake huyo (Hassan Moshi), baada ya kumtambulisha ugomvi ndio ukaanzia hapo. Watonyaji wa habari hiyo wakasema Hammer Q alianza kumpa kichapo mkewe huyo ambaye alikuwa yupo kwenye maandalizi ya sherehe ya kitchen Party yake ambayo ilikuwa ifanyike Tarehe 24/05/2013 ingawa harusi ilikuwa tayari imeshafanyika.
Baada ya Songombingo hilo kutulizwa na washkaji zake Hammer Q wanandoa hao wakatulia, wakashiriki shughuli hiyo ya uzinduzi mpaka ilipoisha na baada ya hapo wakaondoka na kuanza safari ya kuelekea nyumbani kwao Magomeni ambako pia wana mji wao ukiachilia kule kigamboni. Kwa mujibu wa Hammer Q anasema alipofika nyumbani mkewe huyo alianza kumsemea maneno ya kashfa na kuanza kumdai talaka na ndio hasira zikampanda na kuanza kumpelekea kipigo cha MBWA MWIZI kwa mujibu wa majirani walioshuhudia tukio hilo, Hammer Q aliendelea kumpiga mkewe huyo kama vile anataka kumtoa Roho, majirani walipokuwa wanaingilia ili kuweza kusuluhisha inasadikiwa Hammer Q akawa anasema anampiga mkewe huyo kwa sababu amemuoa na amemgaramia, tukio hilo la kikatili lilidumu takribani nusu saa mpaka pale wasamaria wema walipofanikiwa kumnasua mkewe huyo katika mikono ya mumewe huyo (Hammer Q) ambaye wadau wengi wanasema ni mchezo wake kuwapa vichapo wale ambao huwa na mahusiano nao kimapenzi kwa kisingizio cha wivu.
Hata hivyo baada ya tukio hilo wasamaria wema walimpeleka Salha (Mke) mpaka hospitali ya magomeni kwa matibabu na kwenda kufungua kesi katika Kituo cha polisi cha magomeni, Wafuatiliaji wetu hawakuishia hapo ikawalazimu wampigie simu Hammer Q kutaka kujua zaidi ana uamuzi gani kutokana na kitendo chake hicho lakini yeye alikiri kufanya kitendo hicho cha kikatili na kuishia kuwaomba samahani watanzania, wanafamilia ya Mkewe huyo pamoja na majirani kwa kusema haikuwa dhamira yake ila ni POMBE tu ndio zilimpelekea afanye kitendo kile.
Familia ya Baba yake Salha (Mke) wametaka Hammer Q akamatwe haraka sana kwa kutenda kitendo cha kikatili ambacho hakikubaliki kwenye jamii ya Watanzania wa karne hii, pia kwa mujibu wa Mke (Salha) amesema Hammer Q alishamwandikia talaka yake kwa maelezo ya talaka tatu ambayo alikata kijikaratasi kimoja na kumwandikia kama talaka, Wadau mtatusaidia kama talaka hiyo ni halali au La!
Taarifa zaidi tutawaletea kama ameshakamatwa au La! ingawa majirani wanasema walipokuwa wanampigia simu alikuwa anasema anataka kujiua kwa kudhani yeye alishakuwa amemuua Salha (Mke) kwa sababu alipokuwa anatolewa nyumbani alikuwa amezimia hajitambui. Salha ameshonwa nyuzi kadhaa kichwani na mkononi.
wakati akihojiwa na GEAH HABIB wa leo tena ya clouds fm, Hammer Q amesema ni shetani tu alimpitia
Story kwa hisani ya 
kapingaz.blogspot.com

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.