Sunday, September 4, 2016

Licha ya kufungwa na Nigeria,Stars yalamba kitita cha milioni 21.7.

Licha ya kupoteza mchezo wake dhidi ya Nigeria kwenye mchezo wa kufuzu kuelekea michuano ya kombela mataifa 2017,Taifa Stars wamevuna kitita cha dola 10,000 kutoka kwa Gavana wa jimbo la Akwa Ibom State,Godswill Akpabio  ambapo ndipo unapopatikana Uwanja wa Uyo uliotumika kwenye mchezo wa jana.
 Gavana huyo alitoa kitita hicho ambacho ni sawa na milioni 21.7 wakati waliokuwa wakipata chakula cha usiku kwa pamoja wachezaji wa Stars baada ya mchezo huo kutokana na mabadiliko ya kiwango kilichooneshwa na  wachezaji wa Stars, ambao walikuwa wakiongozwa na nahodha wao Mbwana Samatta ambaye kabla ya mchezo huo alikuwa gumzo kwa Wanigeria ambao wamekua na rekodi ya kifunga Tanzania kwenye michezo yote.
Hata hivyo,wachezaji ambao walionesha kiwango kikubwa sana kilichowapa mashaka Nigeria ni pamoja na Aishi Manula, Simon Msuva na mabeki wa kati Vincent Andew na David Mwantika ambapo Gavana huyo pia aliwapa wachezaji wa timu ya Nigeria Naira mil 10 kama pongezi kwa ushindi wao waliopata na kuahidi kuwapa zaidi endapo watafanikiwa kupata nafasi ya kushiriki fainali za Kombe la Dunia mwaka 2018 nchini Russia.
                                                Gavana Godswill Akpabio.

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.