Kutoka Kushoto ni TID, Ray C na Q Chila ambaye naye aliwahi kujitangaza kuwahi kutumia madawa ya Kulevya na kuacha |
Inasemekana Ray C ali coment kwenye Post ya TID Instagram kwa kumwambia msanii huyo amtafute, kauli ambayo Tid aliichukulia tofauti na kuanza kumshushia maneno mazito
Kwa mujibu wa TID anasema kama kweli Ray C alikua ana shida na yeye kwanini amwandikie kwenye Mitandao? kama anataka kulala naye yeye TID hatakiiii kwani Ray C ni Bad Influence na yeye hataki kufundishwa Tabia Mbayaa, na kuongeza kuwa eti hajaonana na Ray C karibu miaka mitano sasa
Nilipompigia simu Ray C kumuuliza kuhusu ishu hii alishindwa kufunguka kwasababu mama anamuuguza mama yake mzazi aliyelazwa hospitali.
Wataalam wa Mambo wanasema eti Ray C alimtafuta Tid eti ili amshawishi kuachana na Madawa, Kheeeee..... kwani TID anatumia?
Kwa watu wanaowafahamu wanadai wasanii hao wanajuana vizuri na eti Ray C alifanya jitihada nyingi kumtafuta TID lakini jamaa alikua hapokei simu.
Sikiliza Interview niliyofanya na TID