Saturday, September 10, 2016

Aliekua Kocha wa Simba SC,James Siang'a afariki dunia.



Kocha wa zamani wa Simba, James siang’a amefariki dunia nyumbani kwake eneo la Bungoma nchini Kenya usiku wa kuamkia leo baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Katibu wa chama cha makocha wa mpira wa miguu nchini kenya (KeFOCA) Bob Oyugi amesema James Siang’a ambaye aliwahi kuichezea Gor Mahia, Luo Union, na timu ya taifa Harambee Stars kama goli kipa amefariki na kuacha pengo kubwa akiwa kama mtu mwenye mchango mkubwa katika soka la Kenya.
  
Siang’a alikuwa golikipa na baadaye akiitumikia timu ya taifa ya Kenya ambapo  lishiriki katika kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 1972 na baadae akawa meneja wa Kenya mwaka kuanzia mwaka 1999 hadi 2000.

Alizidi kung’ara na kuingia nchini Tanzania ambapo alikuwa meneja wa Taifa Stars mwaka 2002, pia amewahi kuwa kocha wa timu mbalimbali katika ukanda wa Afrika mashariki kama Simba SC, Moro United na Express ya uganda .
Mashabiki wa Simba SC watamkumbuka zaidi Siang’a kama Kocha wa mwisho kutamba na Simba kwenye ligi ya mabingwa Afrika hadi sasa ambapo simba ilicheza na Zamaleck na kuifunga goli moja kwa bila mwaka 2003 na kuivua ubingwa klabu hiyo ya Misri ambapo hakuna kocha aliyevunja rekodi hiyo.

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.