Saturday, September 10, 2016

Yanga yazinduka na ushindi wa 3-0 dhidi ya Majimaji.


Baada ya kubanwa na Ndanda FC kwa kulazimishwa suluhu mkoani Mtwara,Yanga imejipoza kwa Majimaji kwa kuichapa magoli 3-0 kwenye mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Uhuru.
Yanga iliandika bao la kwanza dakika ya 35 kipundi cha kwanza likifungwa na Deus Kaseke akiunganisha mpira wa mkwaju wa penati ya Msuva uliogonga mwamba.

  Amis Tambwe amefunga magoli mawili,ambapo alifunga bao la kwanza lake la kwanza dakika ya 75 baada ya golikipa wa Majimaji kupangua krosi ya Msuva kisha Mrundi huyo akausukumia kambani kwa kichwa. Dakika 10 baadae Tambwe alipachika bao lake la pili akiitendea haki krosi ya Juma Mahadh.




 Matokeo ya michezo mingine.
Mbeya City 1-2 Azam
Ruvu Shooting 1-0 JKT Ruvu
Mwadui FC 2-2 Stand Unied
Ndanda FC 0-0 Kagera Sugar

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.