Monday, September 19, 2016

Baada ya Man-United kukubali kichapo,Madee ajibu post ya Pogba Instagram.

Klabu ya Manchester United  kwa mara ya tatu mfululizo katika kipindi cha juma moja imepoteza michezo yake tena ikikubali kufungwa na klabu ya Watford kwa magoli 3-1.

Watford walikuwa wa kwanza kupata goli lilifungwa na Daryl Janmaat kabla ya Marcus Rashford kusawazisha.Ila kiungo wa Watford Zuniga alifunga ikiwa imesalia dakika saba mchezo kukamilika kabla ya Deeney  alifunga penalti katika muda wa ziada baada ya Marouane Fellaini kumchezea vibaya katika eneo la hatari.

Hii ni mara ya tatu mfulilozi kwa Manchester United kupoteza,ikishindwa 2-1 na Manchester City,baadaye ikapoteza 1-0 dhidi ya klabu ya feyenoord ya Uholanzi katikati ya wiki katika kombe la bara Ulaya.

Mara baada ya mchezo huo kumalizika Mshambuaji wa Manchester United,Paul Pogba ali-post ujumbe kupitia ukurasa wake wa Instagram akiwashukuru mashabiki wa United na kuwataka kuwa wavumilivu katika kipindi hiki cha mpito hali ilipelekea mashabiki wengi kuponda ujumbe wa mshambuliaji huyo aliesajiliwa kwa kiasi cha $105m.

Miongoni mwa walitupa madongo kwa mshambuliaji huyo ni Mwanamuziki wa Bongo fleva,Madee Ali  ambae ni shabiki wa Unite alie-coment kwa kuandika "U can wapi ww rudisha mapene ya watu..ww mtu gani ufungi..mbona xhaka kafunga jana".Aliandika Madee.


 Swali la kujiuliza,kwa lugha aliyotumia Madee ujumbe utakua umefika kweli...!!!.


Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.