Sunday, September 11, 2016

VIDEO:Jose Mourinho awatupia lawama mastaa wake.

Kocha wa Manchester United,Jose Mourinho amewalaumu wachezaji wake  akidai  kuwa wao  ndiyo sababu ya kupoteza mchezo wa jana dhidi ya mahasimu wao Manchester City kwa mabao 2-1.

                                                     Jose Mourinho.

Man United walijikuta wakipotezwa kabisa na vijana hao wa Pep Guardiola kwenye dimba lao la Old Trafford, na kujikuta wakiruhusu magoli mawili yaliyofungwa na Kevin De Bruyne na Kelechi Iheanacho.

 Baada ya mchezo huo Mourinho alisema: "Wakati mwingine wachezaji huwavunja moyo mameneja wao".Alimwambia ripota wa Sky Sports.  “Kipindi cha kwanza walikuwa vizuri zaidi yetu"....."Tulianza mchezo huku baadhi ya wachezaji wakicheza chini ya kiwango chao cha kawaida kuanzia kwenye suala la umakini mpaka kasi ya mchezo".

              Jose Mourinho (L) na Meneja wa Man-City,Pep Guardiola wakati wa mchezo.

"Unahitaji kuwa na maamuzi ya haraka namna unavyocheza na unavyofikiri"..."Mchezaji mmoja au wawili hivi walikuwa hawapo kwenye kiwango kizuri na hali hiyo imeigharimu timu".Aliongeza Kocha huyo mwenye tambo nyingi.

Mourinho aliwaanzisha Jesse Lingard na Henrikh Mkhitaryan kwenye kikosi cha kwanza lakini aliwatoa wote baada ya kipindi cha kwanza kuisha baada ya kuonesha kiwango kisichoridhisha

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.