Tuesday, September 6, 2016

VIDEO:Ni kweli kuwa Michel Jackson yupo hai..?

Ulimwengu wa muziki ulitikisika mnamo June 2009 mara baada ya kifo cha Mwanamuziki maarufu na Mfalme wa Pop Michel Jackson huku kifo chake kikidaiwa kusababishwa na matumizi ya dawa za usingizi uliopitiliza ikiwa ni  wiki tatu kabla ya kuafnyika kwa onesho lake lilifahamika kama "This Is It" lililopangwa kufanyika jijini London.

Sasa ni miaka sita tangu MJ afariki ila mjadala wa kifo chake wiki hii ulitawala kwenye baadhi ya mitandao ya kijamii nchini Marekani mara baada ya kusambaa kwa picha ya mtoto wa kike wa Mwanamuziki huyo Paris Jackson (18) ikimuonesha akiwa kwenye gari huku kwenye siti ya nyuma ikionekana taswira tata ya picha ya mtu anadaiwa kuwa na baba yake yaani Michel Jackson,picha ambayo aliifuta baada ya muda mfupi.
 Kwa kudhirihirishwa kuwa Mwanamuziki huyo bado anaishi kwenye mioyo ya watu,baadhi ya mashabiki wake  walichukua picha hiyo na kuitengeneza  video sambamba na picha hiyo wakiamini Mfalme wa huyo wa Pop yupo hai na kuwavutia zaidi ya watazamaji 348,000.
Kwa mujibu wa mtandao wa Mirror,mjadala mzito ulitawala kwenye mitandao ya kijamii huku baadhi ya watu wakioneshwa kuchukizwa na kitendo cha binti huyo kupost picha hiyo tata  huku wengine wakihisi huenda picha hiyo ina ukweli ndani yake.



Baadhi ya Mashabiki waliandika :

'Who's that in the backseat???'  

'I told everyone that he was alive but no, no one believed me! And now they know he's alive!' 
'She's not stupid enough to post this picture if he was really alive.'   

'How many people get fooled by silly hoaxes on the net!'
 
Hata hivyo taarifa zinaonyesha kuwa sio mara ya kwanza kutokea jambo la aina hii kwani mwezi May mwaka huu ilisambaa video nyingine iliyojumuisha picha mbalimbali za Mwanamuiki huyo ikimuonesha mwanamuziki huyo na kundi la watu kwenye matukio tofauti.
Mpaka sasa Familia ya Mwanamuziki huyo haijazungumzia chochote juu ya picha hiyo hii ikimaanisha kuwa taarifa hizo ni uzushi wa mitandaoni. 




Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.