Sunday, November 6, 2016

Dawa ya Wanawake kujifungua bila uchungu yagundulika.

Vitabu vya dini vinasema, mwanamke atazaa kwa uchungu. Lakini wanawake wa siku hizi  hawataki na wanaogopa kuzaa kwa uchungu hali iliyopelekea Madaktari kufanya utafiti na kutafuta  dawa na njia mbalimbali kuhakikisha kuwa Mama mjazito anajifungua kwa raha mustarehe.


Wapo wanawake wengine ambao wanadiriki kuwaomba madaktari wawazalishe kwa kisu mara tu mtoto anapotimia ili mradi kukwepa maumivu ya uchungu ambayo mama hukumbana nayo wakati wa kujifungua.

Wakati wanawake wakiamua kuzaa kwa njia ya upasuaji ili kukwepa maumivu ya mtoto kutoka tumboni, wanasayansi nao wamegundua njia mbadala ya kumfanya mwanamke asihisi uchungu wakati wa kujifungua hii ikiwa ni baada ya utafiti kuonesha kuwa  nyoka mwenye sumu kali zaidi duniani huenda akawa jibu la kupatikana kwa dawa ya kupunguza uchungu.

Nyoka anayeitwa ‘Blue Coral’ ndiye mwenye sumu kali zaidi na hupatikana zaidi Kusini Mashariki mwa Bara la Asia. Utafiti mpya uliochapishwa kwenye jarida la afya la 'Toxin' umesema nyoka huyo huwalenga maadui wake wakiwemo nyoka wenzake,ambao husababisha uchungu kwa binadamu.



Wanasayansi kupiatia utafiti wao wakiongozwa na Dkt.Brian Fry  research of Dr. Brian Fry wanasema huenda sumu hii ikatumika kutengeneza dawa ya uchungu. Baadhi ya wanyama ambao sumu yao imetumika kutengeneza dawa za aina hii ni pamoja na Konokono wa baharini na Bui bui wa sumu.

Wanasayansi sasa wanataka nyoka huyu kuhifadhiwa hususani baada ya maeneo mengi anakopatikana kugeuzwa kuwa mashamba ya michikichi.

 Wanasayansi walifanya utafiti wao katika nchi za China, Singapore na Marekani ambapo hao wanadai kuwa  japo kwa mwanadamu nyoka huwa adui, lakini wakati huu huenda akawa suluhu la matatizo mengi ya kiafya.

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.