Wednesday, August 17, 2016

Picha Tatu Alizopost Idris Sultan Dakika Chache Kabla Ya Kujiondoa Instagram


Kupitia Instagram ndugu yetu Idris Sultan amefanya kile kilichotafsriwa kama kisasi kwa shemela wetu Wema Sepetu ambae siku ya jumatatu alipost picha ya mastaa tofauti huku akiwataja kama #MCM's wake (Yaani Wanaume Wanaomvutia)  akiwemo zilipendwa wake "Diamond Platnumz" aka Bba Tiffah. kama unavyoona hapa chini.

Sasa jana jumatano Idris nae akaitumia siku hiyo kumpost yule aliyemtaja kama #WCW wake huku akisindikiza na hashtag yake #TusichukulianePoa.
 Idris alipost picha tatu za mrembo huyo huku akiahidi kutopost tena kwenye mtandao kwa siku ya jana.

                                       Mapichapicha hayakuishia hapo

 Idris aliendelea kumnadi #WCW wake huku akiendelea kuipa nguvu hashtag yake #TusichukulianePoa

Idris alimaliza kwa post hiyo na muda mfupi baadae ikasemekana Idris Sultan amefuta akaunti yake ya Instagram, Snitch wetu hakutaka kukubali ikabidi aende kwenye page ya Idris ili kujiaminisha alichosikia na haya ndiyo majibu aliyokutana nayo.

Kaa karibu na Gazeti La Makorokocho kwa taarifa zaidi.







ANGALIA HAPA VIDEO MPYA YA SAMATA A- KODO

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.