Sunday, October 9, 2016

VIDEO:Wanafunzi wa kidato cha tatu wakamatwa wakivuta Bangi na kunywa "Viroba".

Katika hali ambayo ni ya kushangaza Walimu wa Shule ya Sekondari Lugalo iliyopo Manispaa ya Iringa kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi kitengo cha Polisi Jamii wameunasa mtandao wa Wanafunzi wa kike na wa kiume wanaojihusisha na uvutaji wa madawa ya kulevya hasa bangi na kunjwa pombe kali aina ya "Viroba" wakati na baada ya vipindi vya darasani.


Msako huo umekuja baada ya Walimu wa Shule hiyo  kuwahisi kuwa huenda wanafunzi wao wanavuta bangi,kutokana na mabadiliko  ya kitabia waliyaonesha Shuleni hapo.

Inadaiwa kuwa Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo baada ya kutoridhika na majibu ya wanafunzi,akaamua kuandaa kikosi cha walimu kwa kushirikiana na Polisi Jamii kufanya uchunguzi kuhusu suala hilo ambapo  baadhi ya wananchi wenye nia njema  walitoa taarifa Shuleni hapo kuwa kuna wanafunzi ambao huwa wanawaona wakivuta bangi kwenye milima iliyopo pembeni kidogo na shule na Shule hiyo.

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.