Thursday, November 3, 2016

Kilichofanya Mahakama iamuru Jide ailipe Clouds Media Group hiki hapa.

Mahakama ya wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, imemkuta na hatia ya Judith ‘Lady Jaydee’ Wambura katika kesi iliyofunguliwa dhidi yake na Clouds Media Group miaka takriban mitatu iliyopita.



Hukumu hiyo imetolewa Jumatano hii (November 2) na Hakimu Boni Lyamike. Katika kesi hiyo, Lady Jaydee alifunguliwa mashtaka na Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Joseph Kusaga pamoja na Mkurugenzi wa vipindi na uzalishaji, Ruge Mutahaba ya kuwachafua/kuwakashfu kupitia blog yake.
Hakimu huyo amemwamuru Lady Jaydee kuwaomba wawili hao radhi kupitia vyombo vya habari kwa kuchafua taswira zao na pia kuwalipa fidia kutokana na madhara waliyoyapata. Jide atatakiwa kulipa gharama za wanasheria ilizotumiwa na Clouds Media kwenye kesi hiyo.
Jaydee aliyekuwa shahidi pekee kwenye kesi hiyo alikiri kuandika maneno ya kuwachafua Kusaga na Ruge kupitia blog yake.
Moja kati ya maneno yaliyomtia hatiani Jaydee ni wosia aliouandika May 2013 kupitia blog yake.

Wosia huo ulioandikwa Jide unasomeka:



Meneja wake, Seven Mosha, ameiambia Bongo5 kuwa Lady Jaydee atatoa maelezo yake kuhusu hukumu hiyo muda si mrefu.
January 8, 2014, Ruge alizungumza kupitia kipindi cha Power Breakfast kuhusu tuhuma mbalimbali alizowahi kutupitiwa na Jide ikiwemo hila za kuipoteza bendi yake ya Machozi.
Alisema anasikitishwa na jinsi Jaydee anavyoendesha harakati zake na kudai kuwa anapigana kwenye vita isiyo sahihi.
  


“Jaydee akaze buti, anapigana na wrong war, vita yake ameidirect tofauti na mizinga yake, bunduki zake amezielekeza kusiko. Skylight Band inamsumbua, akubaliane na ukweli kwamba Skylight ndio iliyoisababishia Nyumbani Lounge kushuka ilivyoshuka, sio Lady Jaydee kama msanii. Vita yake na bunduki zake azielekezee Skylight Band. Hajazungumza hata mara moja kwamba ndio kitu kinachosumbua. Mimi naamini kabisa akifanya hiyo kazi, Jaydee bado ni msanii mzuri, ana nguvu, afanye kazi kubwa ya kuweza kurudisha mapambano yake kisanii, kufanya kazi na aangalie tatizo lililotokea Nyumbani Lounge labda anaweza akatatua matatizo lakini sio kushambulia watu kwenye mitandao,” alisema Ruge.

Pia alisema yupo tayari kukaa meza moja na Lady Jaydee kuzungumza na kumaliza tofauti zao.
“Mimi niko tayari, kesho, kesho kutwa, kama yupo tayari na ana watu wengine wengi tu ambao wanahisi kuna matatizo binafsi ya kuongea na Clouds, twende sehemu nyingine neutral tu, tukodishe, tukae pale tusikie matatizo. Haisaidii muziki wetu kuonekana Bongo Flava ni watu ambao kutwa ni kulalamika, kutwa ni maneno na matusi tu pale panapokuwa na matatizo.”

Credit @skyworkertz


Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.