Thursday, November 3, 2016

VIDEO:Mbowe azua tafrani Bungeni na tuhuma za Wabunge wa CCM anaodai wamehogwa milioni 10 kila mmoja.

Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni Freeman Mbowe katika kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu leo amedai kuwa, mnamo siku ya Jumanne tarehe 25/10/2016 saa mbili usiku kiliitishwa kikao cha wabunge wa CCM ambacho Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alikuwa Mwenyekiti, na kilihudhuriwa na Katibu MKuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, kwa ajili ya kujadili Muswada wa Habari.

Mbowe amesema kuwa Wabunge wakiwemo Mawaziri walihongwa shilingi milioni 10 kila mmoja ili waweze kusaidia kupitisha Muswada wa Habari unaotarajiwa kuwasilishwa Bungeni ili kujadiliwa.



Hata hivyo,Naibu spika alikataa katakata Waziri mkuu kujibu swali la Mbowe kwa waziri mkuu kuhusu tuhuma hizo za wabunge wa CCM kuitwa kwenye kikao na kupewa fedha kiasi cha milioni 10 kila mmoja ili wasiibane serikali kwenye muswada wa sheria unaotarajiwa kuwasilishwa tarehe 4 Mwezi Novemba,2016.

Maelezo ya Naibu spika ni kuwa swali hilo halihusu sera, huku Mbowe akidai linahusu sera kwa kuwa tuhuma hizo ni za rushwa kwa wabunge.

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.