Tuesday, September 13, 2016

Historia ya Rais wa Ufilipino aliemtusi Rais Obama kwa kumwita mtoto wa kahaba.

Rodrigo “Digong” Duterte ni kiongozi ambaye msimamo wake na matamshi yake huzua utata mara kwa mara. Amegonga vichwa vya habari tena baada ya kuonekana kumtusi Rais wa Marekani Barack Obama na kumuita “mwana wa kahaba”.

Duterte aliweza kukabiliana na utata juu yake na kupata ushindi wa kishindo katika uchaguzi wa Ufilipino wa mwezi Mei.


 Baada ya kula kiapo cha urais, Juni 30 Bw Duterte, ambaye kipindi kirefu aliishi mjini Davao kusini mwa nchi tangu aliposhinda, ana mamlaka ya kuongoza taifa hilo kwa muhula mmoja wa miaka sita.

Rodrigo “Digong” Duterte alizaliwa mnamo mwaka 1945 katika familia iliyojikita katika siasa za ndani ya nchi ambapo kwa wakati mmoja baba yake alikuwa gavana wa jimbo na huku familia yao ikitajwa kuwa na uhusiano na familia zenye ushawishi mkubwa za Duranos na Almendrases katika jimbo Cebu, ambako baba yake aliwahi kuwa meya.

Bw Duterte amesomea taaluma ya sheria na alipanda cheo hadi kuwa mwendesha mashtaka kabla ya kuteuliwa kuwa naibu meya wa Davao wakati wa mapinduzi yaliyomuondoa madarakani Ferdinand Marcos mwaka 1986.

 Wafuasi wa Duterte wanasema sifa yake ya ukali ndio wafilipino wanayohitaji ili kukabiliana na ufisadi na uhalifu.
 
Alijijengea umaarufu kwa kupiga vita baadhi ya matatizo makubwa yanayowakabili Wafilipino – uhalifu, makundi ya uasi, na ufisadi. Yote haya yalipungua kwa kiwango kikubwa wakati alipokuwa kiongozi wa Davao, na kufanya mji huo kuwa mmoja wa miji salama zaidi nchini Ufilipino.

Alikuwa meya mwaka 1988 na kushikilia wadhfa huo kwa kipindi cha miaka 10, kabla ya kushinda kiti cha ubunge katika Bunge la Congress kisha akarejea kwenye kiti cha umeya mwaka 2001.Duterte ambaye utawala wake ni wa kipekee,anaelezewa kama kiongozi mwenye sera za Kijamaa na mwanamageuzi ambae sera zake za uchumi zilikuwa si za kuaminika wakati wa kapeni zake.

 Utawala wake na misimamo yake.

Aliahidi kubadili mfumo wa utawala wa taifa kutoka kwa mfumo wa bunge moja kuu yenye hadi kwenye mabunge ya majimbo, ili kugawana vyema mali ya taifa.
Msemaji wake alisema kutakuwa na “mageuzi makubwa yatakayofanyiwa katiba ya nchi”.
Pia alikuwa ameahidi “kuwaua wahalifu 100,000” akiingia ikulu na kudai kuwa atatoa ruhusa kwa vikosi vya usalama mamlaka ya  “kupiga risasi na kuuwa” washukiwa wa uhalifi  wanaokwepa kukamatwa hasa wale wa madawa ya kulevya.
Tayari kufikia sasa, washukiwa 2,5000 wameuawa.

 Tabia yake ya kuwatusi watu.

Amewahi kutangaza hadharani kwamba Ufilipino, ambayo imekuwa mshirika mkuu wa Marekani, haitategemea sana Washington.
Kijamii, yeye huunga mkono wapenzi wa jinsia moja lakini ni mhafidhina katika masuala mengi ya kijamii. Amegusia kupiga marufuku unywaji pombe maeneo ya wazi na kutoa amri ya kutotoka nje kwa vijana.
Amekuwa akiwatusi watu mashuhuri. Alimwita Papa Francis “mwana wa kahaba” huku akijua wazi kuwa Ufilipino ni taifa lenye Wakatoliki wengi.Amewahi kumtusi pia waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry kwa kumuita “mwendawazimu” na majuzi alimweleza balozi wa Marekani nchini Ufilipino kama “mpenzi wa jinsia moja ambaye ni mwana wa kahaba”.
Alifanya mzaha na kusema kwamba alipokuwa meya angekuwa mtu wa kwanza kumbaka mmishenari kutoka Australia aliyeuawa wakati wa fujo gerezani.


 Kuwaua wanawe.

Alisema kwenye mdahalo wa televisheni kwamba anaweza kuwauwa wanawe kama watatumia mihadarati.
Yote hayo yamemuongezea sifa miongoni mwa wananchi wengi nchini Ufilipino kama mtu anayeweza kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha mambo muhimu yanatekelezwa .
Amekuwa akilinganishwa na mgombea wa urasi wa Marekani Donald Trump, lakini alikataa kufananishwa naye,akisema kwamba Trump ni mtu asieshaurika.
Bw Duterte ameoa mara mbili, ana watoto wanne, na miongoni mwao binti yake Sara – alikuwa meya kwa muhula mmoja kabla ya kurejea tena kwa baba yake .
Kwa sasa hana mke, lakini anadai kuwa na marafiki kadhaa wa kike.
 
Chanzo:bbcswahili.
 

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.