Tuesday, September 13, 2016

Wabunge washauri kuhalalishwa kwa matumizi ya bangi kwa sababu za kiafya.

Kundi moja la wabunge nchini Uingereza limetoa wito wa kuhalalishwa kwa matumizi ya bangi kwa sababu za kimatibabu nchini humo.
Kundi hilo linalojumuisha wabunge kutoka vyama mbalimbali vya kisiasa, na ambalo limekuwa likitetea mageuzi kuhusu matumizi ya dawa, limesema kuna ushahidi wa wazi kwamba matumizi ya bangi ya manufaa katika kutibu baadhi ya matatizo ya kiafya, yakiwemo maumivu makali na pia kuondoa wasiwasi.
Wabunge hao wanasema tayari maelfu ya watu huvunja sheria kwa sasa na kutumia bangi kama dawa. Na kwasababu inasaidia hawaoni tabu kufanya matumizi hayo ya bangi kuwa halali. Na iwaruhusu madaktari kutoa ushauri wa kutumia bangi endapo mgonjwa atakuwa na uhitaji.
Aidha, Wizara ya Mambo ya Ndani nchini humo imesema kufikia sasa hakuna mipango ya kuhalalisha matumizi ya “dawa hiyo hatari”.
Taasisi ya Taifa ya Afya nchini Uingereza imetahadharisha wananchi kwamba bangi ina madhara makubwa kwa mwili, ikiwemo uwezo wa mtu kuendesha gari kupungua na vile vile inaathiri mapafu na afya ya akili, huathiri uwezo wa mtu kuzaa na mbaya zaidi bangi huathiri watoto ambao bado hawajazaliwa.
Asilimia   (9%) ya watu wanaotumia bangi mpaka sasa ni watu tegemezi, japo ndiyo si asilimia kubwa kulinganishwa na watu wanaotumia tumbaku (32%) na wale wanaotumia pombe kama kilevi (15%). Na kutahadharisha idadi hiyo huenda ikaongezeka endapo bangi itahalalishwa.
Licha ya yote hayo, wabunge hao wanasema wametathmini na kupata ushahidi kutoka kwa wagonjwa 623. Na vile vile waliweza kuzungumza na wataalamu kutoka nchi nyingi duniani na wamegundua bangi inaweza kufaa sana kama dawa. Matumizi ya bangi kwa sababu za kimatibabu yamehalalishwa katika majimbo 24 nchini Marekani na pia nchi kama Canada na Israel wao pia wameshahalalisha. Huku nchi zaidi ya 10 duniani kwa sasa wamesharuhusu matumizi  ya bangi kwa sababu za kiafya. 

Chanzo– BBC

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.