Sunday, October 23, 2016

UKAWA wasusia uchaguzi wa Meya Kinondoni,Wagombea wa CCM wapita bila kupigwa.




Madiwani wa vyama vinavyounda umoja wa  UKAWA wamesusia uchaguzi wa Meya na naibu meya wa Halmashauri ya manisapa ya Knondoni,uliofanyika Oktoba 23,2016 hali iliyopelekea wajumbe wa chama cha mapinduzi (CCM) kuwapigia kura wagombea wao bila upinzani.

Wabunge hao wa upinzani wamesusia uchaguzi huo wakinukuu sheria ya vyama vya siasa ya mwaka 1992, na sheria ya serikali za mitaa ya mwaka 1982 ambazo  haziruhusu wabunge zaidi ya watatu walioteuliwa na Rais kupiga kura kwenye Halmashauri moja.

Wabunge waliolalamikiwa ni pamoja na Prof.Joyce Ndalichako na Balozi Dr.Augustino Mahiga ambao waliapishwa kama madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala.

CCM wamemchagua Benjamini Sitta kuwa Meya wa Manispaa hiyo kwa kura zote 18 za wajumbe wa chama hicho ambapo George Manyanya amchagiliwa kuwa Naibu Meya.

Comments System

facebook

Disqus Shortname

Powered by Blogger.